• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Ziara ya Kamati ya Siasa Wilaya Busega yatembelea Miradi ya Maendeleo; Kwa kiasi kikubwa yaridhishwa na Utekelezaji

Posted on: June 20th, 2021

Kamati ya Siasa Wilaya ya Busega imetembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani Busega. Ziara hiyo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Daudi Ng’hindi imefanyika kwa siku mbili, kuanzia tarehe 18 hadi 19 Juni, 2021. Katika ziara hiyo Kamati ya Siasa imeweza kutembelea miradi ya sekta ya elimu, maji, afya, na kwa sehemu kubwa imeridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo.

Katika ziara hiyo, Kamati ya Siasa imeweza kutoa maelekezo kwa wasimamizi wa miradi kwa lengo la kuleta ufanisi wa utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali. Katika ziara hiyo Kamati ya Siasa imetaka kuwepo kwa mambo muhimu yafuatayo;

  • Kuanza kutumika kwa miradi yote ambayo imekalika ili wananchi wapate huduma.
  • Kuweka kipaumbele cha miundombinu ya watu wenye mahitaji maalum katika vituo vya afya na mashuleni.
  • Kusimamia vyema na kufuatilia kwa ukaribu miradi ili kuwa na ubora wa miradi mbalimbali inayotekelezwa.

Elimu 

Miradi liyotembelewa katika sekta ya elimu ni mradi wa ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa  na ofisi 1 Shule ya Msingi Mirambi kwa gharama ya TZS Milioni 30, ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa Shule ya Msingi Mwanangi kwa gharama ya TZS Milioni 60, madarasa yamekamilika na yanatumika, ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa Shule ya Sekondari Nyaruhande kwa gharama ya TZS Milioni 21.3, ujenzi wa maabara Shule ya Sekondari Gininiga kwa gharama ya TZS Milioni 13, ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa Shule ya Msingi Fogofogo na matundu 7 ya vyoo kwa gharama ya TZS Milioni 47.7, ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa Shule ya Sekondari Kabita kwa gharama ya TZS  Milioni 40, ujenzi umekamilika, ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na matundu 7 ya vyoo Shule ya Msingi Itongo kwa gharama ya TZS Milioni 47.7 ujenzi umekalika, ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na matundu 7 ya vyoo Shule ya Msingi Mwamajashi kwa gharama ya TZS milioni 47.7, ujenzi umekamilika.  

Afya 

Ujenzi wa wodi tatu za wanaume, wanawake na watoto Hospitali ya Wilaya ya Busega, ambapo Serikali imetoa kiasi cha TZS Milioni 500. Ujenzi wa majengo hayo unaendelea. Ujenzi, ukarabati wa vyoo na uwekaji wa miundombinu ya maji Kituo cha Afya kiloleli kwa gharama ya t TZS Milioni 27, ujenzi, ukarabati wa miundombinu ya vyoo vya Watumishi na uwekaji wa miundombinu ya maji Zahanati ya Badugu kwa gharama ya TZS Milioni 20, ujenzi wa vyoo vya wagonjwa na watumishi na uwekaji wa miundombinu ya maji kwa gharama ya TZS Milioni 20 Zahanati ya Ngasamo, ujenzi wa vyoo vya watumishi na uwekaji wa miundombinu ya maji Zahanati ya Shigala kwa gharama ya TZS Milioni 20, ujenzi wa vyoo na uwekaji wa miundombinu ya maji kwa gharama yaTZS Milioni 25, ujenzi wa miundombinu ya vyoo na uwekaji wa miundombinu ya maji Zahanati ya Kijesrishi kwa gharama ya TZS Milioni 20.

Maji 

Ujenzi mradi wa tanki la maji Mkula wenye thamani ya TZS Bilioni 2.1 ambapo tanki hilo lina ukubwa wa lita 300,000. Ujenzi unaendelea na mpaka sasa ujenzi umefikia asilimia 60, ukamilikaji wa mradi huu utahudumia watu 16,108 ambapo vituo 33 vitajengwa kwaajili ya huduma ya maji Wakazi wa Mkula, Lutubiga na Kijerishi.

Pia kamati hiyo imeweza kutembelea ujenzi wa mradi wa maji Mwamanyili ambao tahamani yake ni TZS Milioni 227.7 ambapo utekelezaji wa mradi huu ni asilimia 45 mpaka sasa. Ujenzi wa tanki wa mradi huo wenye ukubwa wa lita 225,000 umekamilika hatua iliyobaki ni kuanza usambazaji maji kwa watumiaji.

Miradi Mingine

Mradi mwingine ambao ulitenmbelewa na ziara hiyo, ni mradi wa ujenzi wa soko la Masanza Kata ya Kiloleli, ambapo kamati ilifika kukagua ujenzi wa choo cha Soko ambacho kimegharimu TZS Milioni 6. Katika ukaguzi wa choo hicho kamati imeagiza Ofisi ya Mkurugenzi kuendelea na jitihada za kuweka miundombinu katika choo hicho ikiwemo maji na umeme ili kuweka mazingira bora pale kitakapoanza kutumika.

Aidha, kamati ya siasa Wilaya ya Busega imeweza kufika katika Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS), ambapo walitembelea AMCOS ya Bushigwamh’ala iliyopo Kata ya Kalemela na AMCOS ya Kijerishi iliyopo Kata ya Mkula, kukagua na kujionea hali ya ununuzi wa Pamba. Kamati hiyo ikiwa katika AMCOS hizo imeweza kupata taarifa kutoka kwa viongozi lakini pia kusikiliza changamoto wanazokutana nazo, hasa wauzaji wa Pamba ili kuzifanyia kazi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Anderson Kabuko amewashukuru wajumbe wa kamati hiyo na kuahidi kutekeleza mambo yote yaliyoelekezwa na kamati hiyo ili kuendelea kuboresha huduma Wilayani Busega kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akihitimisha ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Busega Mhe. Daudi Ng’hindi, amesema ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kikamilifu ni muhimu kuwa na ushirikiano katika kutekeleza miradi hiyo, na kuzingatia maelekezo yanayotolewa.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa