• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WENYEVITI NA MADIWANI WAANZA KULIPWA POSHO ZAO BUSEGA

Posted on: April 7th, 2018

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mhandisi Mohamed Yamlinga amesema posho za wenyeviti wa vijiji na vitongoji wa Wilaya ya Busega tayari zimeanza kulipwa.

Yamlinga ameyasema hayo katika baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Busega lililofanyika mapema mwishoni mwa wiki hii katika ukumbi wa SILSOS uliopo katika kata ya Nyashimo wilayani hapa. Aliendelea kulieleza baraza kuwa Halmashauri inaendelea kufanya juhudi za kina ili kuhakikisha malimbikizo yote ya posho yanalipwa ndani ya kipindi kifupi.

Naye mhasibu wa mapato ya ndani ya Halmashauri, Bwana Gumuka Misambo, amesisitiza kuwa tayari kiasi cha Shilingi 4,182,000 kwa kata ya Kalemela, Kiloleli, Lamadi,Igalukilo na Nyaluhande kimeishalipwa huku kiasi cha shilingi milioni 40 kimeishalipwa kwa waheshimiwa madiwani kupitia benki ya CRDB. Gumuka ameendelea kulieleza baraza kuwa kumekuwa na changamoto sana wakati wa kuwalipa posho kwani mara nyingi wanakuta akaunti zilizofunguliwa na kata ni ‘dormant’ hivyo kufanya zoezi la ulipaji kuwa gumu.

Aidha, afisa Kilimo wa Wilaya ya Busega Bwana Juma Chacha  amesema kuwa pembejeo zilishasambazwa kwa wakulima wa Wilaya hii ingawa baadhi wa wakulima hufanya uzembe na kukaa muda mrefu bila kwenda kuchukua pembejeo hizo na kusababisha uharibifu baada ya kukaa muda mrefu, Bwana Chacha ametoa maelezo hayo baada ya mjumbe wa baraza kutaka kujua kama pembejeo ziishaanza kusambazwa kwa wakulima. Chacha ameshauri wakulima kujitokeza mara moja kuchukua pembejeo mara tu zinapoletwa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Tano Mwera amesisitiza wananchi wote kuwaandikisha watoto wao walio na umri wa chini ya miaka mitano (5) katika vituo vya kusajili watoto ili wapewe vyeti vya kuzaliwa kwani ni haki ya watoto kupata vyeti hivyo.Pia Mhe. Tano amesisitiza vikao vya baraza visichukue siku nzima na badala yake vifuate taratibu, kanuni na sheria zilizowekwa.

Katika Hatua nyingine, Mwakilishi kutoka katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bwana Maganga amewahasa waheshimiwa madiwani wote kuwa na njia mbadala za kuhakikisha kunakuwa na viwanda vidogo vidogo katika kata zao ili kuunga mkono juhudi za Serikali hii ya awamu ya tano ya uanzishwaji na uboreshwaji wa viwanda vya ndani. Maganga amesisitiza kuwa viwanda hivyo vitasaidia kukuza uchumi wa nchi na kutoa ajira kwa wananchi.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa