• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

wavuvi na Wakazi wa Nyamikoma wapewa Elimu ya Ufugaji Samaki kwa kutumia Vizimba

Posted on: January 13th, 2021

Elimu ya ufugaji Samaki kwa kutumia Vizimba imetolewa kwa Wavuvi na Wakazi wa kijiji cha Nyamikoma kilichopo kata ya Kabita wilayani Busega mnamo tarehe 11 Januari 2021. Elimu hiyo imetolewa huku ikiwa ni ombi la Wavuvi kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Mashauri Ndaki alipotembelea kijiji hicho na kufanya mkutano mnamo tarehe 30 Disemba 2020.

Katika kuhakikisha Serikali inaitikia kilio cha wavuvi na wakazi wa kijiji cha Nyamikoma, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeweza kutuma mwakilishi ili aweze kutoa elimu ya ufugaji wa Samaki kwa kutumia vizimba ili wavuvi waweze kupata uelewa wa kufuga Samaki kwa njia ya kisasa. Miongoni mwa mambo muhimu yaliyoelezwa na Afisa kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Silas William ni pamoja na maeneo yanayofaa kwa kuweka vizimba, jinsi ya kutengeneza vizimba, aina ya vyakula vinavyotakiwa kulisha vifaranga vya Samaki, ukubwa wa vifaranga wanaotakiwa kufugwa na taratibu muhimu za kupata kibali cha ufugaji wa Samaki.

Aidha Bw. William amesema ufugaji huu una umuhimu mkubwa kwa uchumi wa mwananchi na kwa nchi kiujumla, huku akisisitiza ya kwamba ufugaji wa Samaki kwa kutumia vizimba katika ziwa Viktoria kwa sasa umelenga kwa ufugaji wa Samaki aina ya Sato pekee kwani ndio waliofanyiwa utafiti kitaalam wanaofaa kwa ufugaji.

Kwa upande mwingine Bw. William aliweza kueleza taratibu muhimu ambazo mfugaji atatakiwa kuzifata ili aweze kufanya ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba ikiwemo kuwa na taarifa ya utafiti wa eneo la kuweka kizimba, kibali cha utumiaji maji, mchoro pendekezwa wa kizimba, na mukhtasari wa serikali ya kijiji husika.

Wananchi wameonesha kuvutiwa na elimu waliyopewa lakini wameomba iwe endelevu ili iweze kuwajengea uwezo zaidi. Kwa upande mwingine wameiomba Serikali kuimarisha zaidi ulinzi ili watakapoanza ufugaji, ulinzi uwe miongoni mwa mambo muhimu kwani wanahofia wizi na muingiliano wa wanyama wengine kama Viboko ambao wamekuwa wakifanya uharibifu mara kwa mara.

Hata hivyo Bw. William amewatoa hofu wavuvi na wakazi wa Nyamikoma kwa kueleza kwamba suala la usalama ni moja ya masuala vipaumbele katika ufugaji huu na ndio maana Wizara ya Serikali inaelekeza kabla ya ufugaji kuanza ni lazima ufanyike utafiti wa kina ili kujua na kutathmini kama eneo linafaa kwaajili ya shughuli za ufugaji, pia kujua kama eneo linalokusudiwa kuwekwa vizimba halitakuwa na muingiliano wowote wa shughuli zozote na muingiliano wowote wa wanyama hatarishi ikiwemo Viboko.

Elimu ya ufugaji wa samaki inatolewa kwa wavuvi na wakazi wa Nyamikoma ikiwa ni mwitikio wa ombi kutoka kwa wananchi wa kijiji hicho kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi alipotembelea Mwalo wa Nyamikoma mwishoni mwa mwaka jana.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa