• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TASAF Mkombozi Kaya Masikini Busega

Posted on: March 20th, 2020

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii wa kunusuru kaya masikini, TASAF umekua nuru ya kukomboa kiuchumi kaya masikini Wilayani Busega. Mpango huu ulianza rasmi kwa kaya masikini kutambulika na ugawaji fedha kwa walengwa mwaka 2015 katika wilaya ya Busega. Jumla ya walengwa 3826 wamefaidika na mradi wa TASAF kipindi cha kwanza awamu ya tatu.

Jumla ya vijiji 41 kati ya 59 vimejumuishwa kwenye mpango wa TASAF kipindi cha kwanza awamu ya tatu na zaidi ya Tshs. Milioni 766 ziligaiwa kwa kaya lengwa. Mpango wa TASAF ni miongoni mwa dhima kubwa na kipaumbele cha kupunguza umasikini kwa kaya masikini nchini Tanzania, hivyo serikali na kaya lengwa zina matumanini makubwa katika mpango huu.

Kuwepo kwenye mpango wa TASAF kwa wilaya ya Busega tangu mwaka 2015 ni ushahidi tosha kuwa mpango huu umekuwa mkombozi wa jamii nyingi masikini wilayani humo. Kaya nyingi zimepata mwangaza wa kujikomboa kutoka kwenye dimbwi la umasikini uliopitiliza kwa kujiwekea malengo fanisi ya matumizi ya pesa wanazopata kwa kuwekeza kwenye shughuli za maendeleo.

Shughuli zenye tija na zenye kuchochea maendeleo zinazofanywa na kaya zinazofaidika na mpango wa TASAF kwa wilaya ya Busega ni pamoja na ufugaji, biashara ndogondogo, kusomesha watoto na shughuli za kilimo. Baadhi ya wafaidika wamekiri kwamba mpango huu wa TASAF ni mkombozi kwao kwakua umefanya maisha ya kaya nyingi kuinuka kiuchumi kwa kujishughulisha na ujasirilimali.

Mratibu wa mpango wa TASAF wilaya ya Busega Bi. Wema Mmari  amekiri kuwa kuna mwamko mkubwa kwa kaya lengwa kwani zimekuwa katika maendeleo ya kiuchumi kwa kuzingatia malengo bora ya matumizi ya fedha wanazopokea. Kata zote 15 zilizopo wilayani Busega zimekuwa katika mpango wa TASAF awamu ya tatu kipindi cha kwanza. Jamii na kaya lengwa zimekuwa zikipata elimu ya kuhakikisha maisha yao yanaboreshwa kutoka katika utegemezi kwa kutumia fedha wanazopata kikamilifu kwa mambo yenye tija ya ushawishi wa maendeleo. Mpango huu wa kunusuru kaya masikini ni chachu ya maendeleo na mafanikio yake tangu ulipoanza umekuwa ni mkubwa sana.

Kwa kuzingatia umuhimu wa mpango huu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. John Pombe Joseph Maguful, amezindua mpango wa kipindi cha pili cha awamu ya tatu wa kunusuru kaya masikini mapema mwaka huu. Mpango ambao unatarajia kugharimu tirioni 2 za kitanzania kwaajili ya kutoa ruzuku kwa kaya masikini nchni.  

Tangu kuanzishwa kwa TASAF nchini Tanzania mwaka 2000 kumekuwa na tija ya kupambana na umaskini kwa kiasi kikubwa maeneo mbalimbali nchini. Hivyo mpango huu ni nuru ya maendeleo kwa nchi nyingi zilizopo kwenye maendeleo ya uchumi wa kati ikiwemo Tanzania. Wachambuzi wa masuala ya kiuchumi wana matumaini kwamba endapo mpango wa kunusuru kaya masikini utaongeza kiwango cha ruzuku  katika kaya, utasaidia Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo 2030.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa