• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa yaridhishwa na Usimamizi wa ujenzi wa Miradi ya Maendeleo Wilayani Busega

Posted on: February 1st, 2022

Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa (CCM) ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Ndg. Daniel Chongolo imefanya ziara ya siku mbili wilayani Busega tarehe 31/01/2022 hadi 01/02/2022 kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo, na kuangalia shughuli za miradi mbalimbali zinazoendelea Wilayani Busega na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo. 


Katika siku ya kwanza ya ziara hiyo Wilayani Busega Naibu Makatibu wa CCM Taifa kwa upande wa Tanzania Bara na Zanzibar Ndg. Christine Mndeme na Ndg. Dkt. Abdalah Mabodi wakimwakilisha Katibu Mkuu walitembelea kukagua mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Mkula na mradi wa vyumba vya madarasa 14 katika shule ya Sekondari Kabita, madarasa yaliyojengwa chini ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19. 


Mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Mkula ambao ujenzi wake unagharimu kiasi cha TZS milioni 400 na ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la upasuaji na jengo la wodi ya wazazi na ujenzi wa majengo hayo unaendelea. Ukamilikaji wa ujenzi wa kituo hicho utahudhumia zaidi ya wananchi 16,800 wa Kata hiyo na wananchi wa maeneo ya karibu. Ujumbe wa Sekretarieti hiyo umeelekeza kwamba huduma zianze tu pale majengo muhimu yatakapokamilika. “Tungependa kuona majengo haya yaanze kutumika tarehe 28/02/2022 kwa majengo yaliyokamilika mkiendelea kumalizia majengo yaliyobaki ili wananchi wa Mkula waweze kupata huduma” aliongeza Mndeme. 


Aidha, Naibu Katibu CCM Taifa upande wa Bara Ndg. Christine Mndeme amewaasa wananchi wa Kata hiyo na Busega kwa ujumla kutumia huduma za hospitali ili kuokoa maisha yao hasa wakina mama. “Tunapaswa kushawishi na kutoa elimu kwa wanachi hasa wajawazito kuja kuhudhuria kliniki na kujifungulia katika vituo vya Afya ili kuokoa maisha ya mama na mtoto” alisema Mndeme. 


Halikadhalika, ziara hiyo ilitembelea mradi vyumba vya madarasa yaliyojengwa chini ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19 katika shule ya Sekondari Kabita ambapo jumla ya TZS milioni 280 imetumika kujenga vyumba 14 vya madarasa. Sekretarieti hiyo imeridhika na ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa ambavyo vimeanza kutumika. Aidha, Mndeme amesema changamoto za vyumba vya madarasa kwa shule za msingi ni jambo ambalo wao kama chama wanaendelea na mikakati ili Serikali iweze kutatua tatizo hilo kama ilivyo kwa shule za sekondari. Kwa upande mwingine ujumbe wa Sekretarieti hiyo imeagiza Halmashauri ya Wilaya ya Busega kuona namna ya kujenga miundombinu katika shule ya msingi Masangani ambayo kwasasa ni shule shikizi.


Katika siku ya pili ya ziara hiyo ujumbe wa Sekretarieti CCM Taifa ilifanya ziara ya kukagua ujenzi wa wodi tatu katika hospitali ya Wilaya ya Busega, ambapo Serikali imetoa kiasi cha TZS milioni 500 kwaajili ya ujenzi wa wodi ya wanaume, wanawake na watoto. Ujumbe wa Sekretarieti ya CCM Taifa iliridhika na mwenendo wa ujenzi wa wodi hizo na kusisitiza kwamba huduma za Afya ziendelee kutolewa kwa ufanisi mkubwa kwani lengo la Serikali ni kufikisha huduma bora kwa wananchi ikiwemo huduma za Afya. 


Ujumbe wa Sekretarieti hiyo umeagiza kuharakisha utengenezwaji na uwekaji wa miundombinu ya maji, barabara na umeme katika hospitali ya Wilaya na vituo vya Afya ili kuwezesha huduma bora za Afya. Pamoja na mengineyo, ujumbe wa Sekretarieti hiyo ulipata muda wa kukutana na kuzungumza na baraza la wazee wa Busega ili kusikiliza kero na changamoto zao zinazowakali na kutembelea mashina ya chama hicho.


Uongozi wa Wilaya ya Busega ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria imetoa shukrani kubwa kwa Sekretarieti ya CCM Taifa. “Tutafanyia kazi yote yaliyoelekezwa ili kuondoa changamoto zilizopo” aliongeza Zakaria. 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa