• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC Kafulila Aipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Busega kwa Usimamizi Bora wa Matumizi ya Fedha

Posted on: June 28th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Busega kwa kupata hati safi iliyotokana na ufanisi katika utendaji wa majukumu mbalimbali ikiwemo usimamizi wa matumizi wa fedha za Serikali. Kafulila amesema hayo wakati wa Baraza Maalum la Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2020/2021, lililofanyika leo tarehe 28 Juni 2022.

“Nawapongeza kwa kupata hati safi nitoe wito kwa uongozi na watumishi wa Wilaya ya Busega kuendelea kuchapa kazi kwa bidii na maarifa ili kutekeleza lengo la Serikali”, amesema Kafulila. Aidha, Kafulila amewataka watumishi wa Halmashauri kuendelea kuwa na morali na kupenda kazi zao ili kuwahudumia wananchi.

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa halamshauri ya Wilaya ya Busega Mhe. Ng’habi Mojo amesema licha ya kuwa na mwendelezo wa kupata hati safi lakini amesisitiza kutobweteka kwa watendaji, kwani hali hiyo inaweza kusababisha matokeo mabaya na yasiyoridhisha.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bi. Veronica Sayore amesema tayari hoja zipatazo 24 zimefanyiwa kazi huku hoja 34 zikiendelea kufanyiwa kazi. Awali, Mkaguzi Mkuu wa nje wa Hesabu za Serikali Mkoa wa Simiyu Gwamaka Mwakyosi amesema katika mwaka wa fedha wa 2019/2020, Wilaya ya ya Busega ilipata maagizo 8 kutoka kwa Kamati ya Bunge ya Ukaguzi wa Serikali za Mitaa (LAAC) na tayari maagizo 3 yamefanyiwa kazi huku mengineyo 5 yakiendelea na utekelezaji wake.

Pamoja na hayo, Kafulila alieleza jinsi alivyoridhishwa na uchapaji kazi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Busega Bi. Veronica Sayore, huku akiwataka viongozi na watumishi wa Wilaya ya Busega kuendelea kushirikiana nae ili aendelee kutekeleza majukumu yake. “Kiukweli nipende kumpongeza Mkurugenzi kwa kuchapa kazi ya hali ya juu hasa kwa upande wa ukusanyaji na matumizi ya fedha kwani mpaka sasa tayari makusanyo ya ndani yamefikia asilimia 97”, aliongeza Kafulila.

Halikadhalika, Kafulila amesema hana budi kumpongeza Mkurugenzi kwa upande wa fedha za miradi ya maendeleo, fedha zinazotokana na mapato ya ndani ambapo mpaka sasa asilimia 99 imepelekwa kutekelezwa miradi mbalimbali, huku akionesha kufurahishwa na utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa makundi ya wanawake, walemavu na vijana kwani Wilaya ya Busega mpaka sasa imetekeleza  kwa asilimia 100.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa