• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC David Kafulila Ataka Uvuvi Kuwa Kichocheo cha Maendeleo Busega; Ataka Mikakati Zaidi Uzalishaji Zao La Pamba

Posted on: June 24th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila ametaka uvuvi kuwa fursa ya kimkakati katika kuchochea maendeleo Wilayani Busega. Ameyasema hayo wakati wa Baraza la Madiwani la Kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka ulioishia 30 Juni 2020 Wilayani Busega, lililofanyika tarehe 24 Juni 2021.

Mhe. Kafulila amesema ni wakati sasa umefika kwa Wilaya ya Busega kuhakikisha inafanya mapinduzi makubwa ili kutumia sehemu ya ziwa Viktoria kuongeza tija ya shughuli za uvuvi. “Mnatakiwa kuhakikisha mnatumia fursa ya uvuvi kuleta kasi ya maendeleo, shughuli ya uvuvi iwe miongoni mwa mikakati muhimu ya Wilaya ya Busega”, aliongeza Kafulila.

Kwa upande mwingine Mhe. Kafulila amesema kipaumbele cha uvuvi na vipaumbele vingine haviwezi kufanikiwa kama hakutakuwa na usimmamizi na muamko wa wananchi. Amewataka wawakilishi wa wananchi, ambao ni madiwani kusimamia vyema Mipango ya Halmashauri kupitia vikao vya mabaraza.”Kuongeza ufugaji wa Samaki kupitia vizimba itaongeza shughuli za uvuvi Wilayani Busega”, alisema Kafulila.

Mhe. Kafulila pia ametaka kuimarika kwa usimamizi wa kilimo cha zao la Pamba, kwani Mkoa wa Simiyu unachangia zaidi ya asilimia 55 ya Pamba yote nchini. Amesisistiza kwamba malengo ya Mkoa kwenye uzalishaji wa zao la Pamba kwa msimu ujao ni kufikia tani 500,000, ambapo itasaidia kuongeza mapato ya Halmashauri za Mkoa wa Simiyu.

Mhe. Kafulila amesema kwamba ili kufikia malengo ya uzalishaji wa pamba kufikia tani 500,000, ni muhimu kuweka mikakati, ikiwemo kuhakikisha kila mkulima wa zao la Pamba anapatiwa mbolea, hasa mbolea ya Samadi. Kwa upande mwingine Kafulila ametaka kusimamiwa vyema uuzaji wa pamba ili kulinda maslahi ya Wakulima, na kusisitiza kutowaonea haya wote watakaobainika kuhusika na wizi wa ununzi wa Pamba.

Awali, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mkoa wa Simiyu Bw. Gwamaka Mwakyosi, amesema Busega imeendelea kupata hati safi, lakini ametaka uzingatiaji wa matumizi bora ya fedha za Serikali ili kuongeza ufanisi wa shughuli mbalimbali.

Akifungua kikao cha Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mhe. Sundi Muniwe, kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi ambae ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu mhe. David Kafulila, aliweza kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria ili ajitambulishe, kwani ni mara yake ya kwanza kuhudhuria Baraza hilo tangu ateuliwe katika nafasi hiyo.

Mhe. Gabriel Zakaria amesema anajisikia furaha kuhudhuria kikao cha Baraza la Madiwani na kusisitiza kwamba amekuja kuwatumikia Wananchi wa Wilaya ya Busega kwani yupo tayari kushirikiana na viongozi wa Wilaya ya Busega.  Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Anderson Kabuko amesema Ofisi yake itayafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa ili kufikia malengo ya Serikali.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa