• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

NINAWAPONGEZA MADIWANI KWA UFUATILIAJI WA SHUGHULI MBALIMBALI ZA MIRADI YA MAENDELEO-GABRIEL ZAKARIA

Posted on: March 4th, 2022

Kutoka Busega

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amewapongeza Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega kwa kazi kubwa ya usimamizi na ufuatiliaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa Wilayani Busega. Zakaria ametoa pongezi hiyo wakati wa kikao cha robo ya pili cha baraza la Madiwani kilichofanyika tarehe 03/03/2022.

“Niwapongeze kwa umakini wenu, maana mmeonesha ni jinsi gani mnafuatilia kwa karibu  shughuli mbalimbali zinazoendelea katika Halmashauri na Wilaya kwa ujumla”, alisema Zakaria. Katika kikao hicho ambacho Madiwani waliweza kuhoji mambo mbalimbali ikiwemo fedha za miradi kwa lengo kupata uelewa na ufafanuzi.

Halikadhalika, Zakaria amewakumbusha Madiwani kuhimiza wazazi kuwapeleka shule watoto ambao wamefikia umri wa kuanza shule. “Tuhamasishe uandikishaji wa watoto mashuleni, kwa watoto wote wanaostahili kuwepo shuleni, hii itasaidia kuongeza idadi kubwa ya watoto katika shule zetu na hii ndio dhima kuu ya Serikali ya awamu ya sita katika sekta ya elimu”, aliongeza Zakaria.

Pamoja na kutambua kazi kubwa inayofanywa na Madiwani, pia Zakaria amewataka Madiwani kuendelea kufuatilia miradi inayotekelezwa katika maeneo yao ili miradi hiyo iwe na ufanisi mkubwa. Aidha, Zakaria amewakumbusha Madiwani kuendelea kuwaeleza wananchi shughuli za miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali katika maeneo yao kupitia mikutano ya hadhara, kwani baadhi ya maeneo kumekuwa na uelewa potofu kuhusu miradi inayoendelea kutekelezwa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Mhe. Sundi Muniwe amesema madiwani wataendelea kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa lengo la kuijenga Wilaya ya Busega. Aidha, kikao cha baraza hilo limeagiza masuala mbalimbali kufanyiwa kazi ikiwemo uharakishwaji wa fedha za miradi mbalimbali ya maendeleo ili miradi hiyo iweze kukamilika kwa wakati.

Pamoja na hayo, baraza hilo limetaka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha madeni ya vibarua wa Halmashuari yanalipwa ifikapo mwisho wa mwezi huu ili kumaliza suala la madeni yanayodaiwa na vibarua hao, ambao wengi wao ni wakusanya ushuru wa Halmashauri.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Gidion Bunto anasema mchakato wa malipo ya vibarua unaendelea na muda wowote watalipwa fedha zao kwani wamekuwa wakifanya kazi kubwa na mchango wao unatambulika. “Tayari tunaendelea na mchakato wa malipo ya vibarua, hivyo watalipwa pale mchakato huo utakapokuwa umekamilika”, alisema Bunto.

Kikao hiki cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kimefanyika ikiwa ni utaratibu wa kila robo katika mwaka wa fedha kwa madiwani kukutana na kujadili shughuli mbalimbali zilizofanyika katika robo husika.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa