• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mwenge wa Uhuru wapitia Miradi ya Maendeleo 7 yenye thamani ya zaidi ya Tshs. Bilioni 1.83 Wilayani Busega

Posted on: July 7th, 2022

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 zinazoongozwa na mkimbiza Mwenge Kitaiafa mwaka 2022 Ndg. Sahili Nyanzabara Geraruma zimepokelewa Wilayani Busega tarehe 06 Julai 2022 ikiwa ni mapokezi ya Mkoa wa Simiyu na kupitia miradi 9 yenye thamani ya zaidi ya Tshs bilioni 1.83 Wilayani Busega. Halmashauri ya Wiliya ya Busega imekuwa halmashauri ya kwanza kukimbiza mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2022 kati ya halmashauri 6 zilizopo Mkoa wa Simiyu, 

Pamoja na kukagua miradi, Ndg. Geraruma ameweza kutoa maagizo ya kuhakikisha miradi ya maendeleo inasimamiwa vyema sambamba na upatikanaji wa nyaraka za miradi yote inayotekelezwa na Serikali na watu binafsi. Aidha, Geraruma amewakumbusha wananchi wa Busega kujiandaa na kushiriki Sensa ya Watu na Makazi ambayo inatarajiwa kufanyika tarehe 23 Agosti 2022. “Tujiandae kushiriki katika Sensa ili kuhakikisha Serikali inapata tathmini ya idadi ya watu kwaajili ya kupanga mipango endelevu”, aliongeza Geraruma.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na mradi wa kituo cha mafuta cha Ndono kilichopo lamadi, mradi ambao una thamani ya Tshs milioni 385, mradi wa kikundi cha vijana cha kufyatua matofali ambacho kinanufaika na mikopo ya halmashauri yenye riba nafuu ambapo kikundi hicho kimepokea kiasi cha Tshs milioni 18.

Aidha, miradi mingine ambayo imepitiwa na Mwenge wa Uhuru ni mradi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya sekondari Shigala, madarasa hayo yamejengwa chini ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19, mradi ukiwa na gharama ya Tshs milioni 60, mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Ngasamo wenye thamani ya Tshs milioni 500, mardi wa maji Kata ya Badugu wenye thamani ya Tshs milioni 369.8,  mradi wa barabara ya Badugu-Lwangwe-Shigala wenye thamani ya Tshs milioni 500.4 na mradi wa klabu ya wapinga Rushwa katika shule ya sekondari Ngasamo wenye thamani ya Tshs 241,000.

Kwa upande mwingine Geraruma ameweza kutembelea mabanda mbalimbali yaliyoandaliwa kwaajili ya kutoa elimu ikiwemo banda la Sensa, banda la Lishe, banda ya TAKUKURU na banda la kupima Virusi vya Ukimwi (VVU) na kupongeza uongozi wa Wilaya ya Busega kwa kusimamia elimu ya kampeni mbalimbali za Kitaifa, hasa elimu ya Sensa.

Wilaya ya Busega imekimbiza Mwenge wa Uhuru kwa umbali wa kilometa 181.5 na kuukabidhi Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Baraidi tarehe 07 Julai 2022 ambapo utakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa