• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria Atilia Mkazo Kuongeza Tija ya Uzalishaji Zao la Pamba

Posted on: July 9th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria ametilia mkazo wa kuongeza tija ya uzalishaji wa zao la Pamba. Mhe. Zakaria Amesema ni wakati sasa umefika kubadilisha mitazamo ya kilimo cha zao la Pamba Wilayani Busega. Ameyasema hayo wakati wa kikao cha majumuisho ya tathmini ya kampeni ya kuongeza tija ya uzalishaji wa zao la Pamba, kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Simba wa Yuda na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali.

Mhe. Zakaria amesema ni wajibu wa viongozi wa Wilaya kusimamia kwa ukaribu shughuli za kilimo cha Pamba ili kufikia malengo ya Wilaya ya kuzalisha tani 50,000 katika msimu ujao wa kilimo. Mhe. Zakaria amewataka Maafisa Ugani kupitia Idara ya kilimo kuhakikisha suala hilo ni moja ya kipaumbele katika majukumu yao, na kusisitiza kwamba atasimamia kwa ukaribu utekelezaji wake. “Nawategemea wataalam wa kilimo, nina imani kwamba Busega tutafikia lengo la kuongeza tija ya uzalishaji wa zao la Pamba kwasababu mmepata mafunzo na kanuni bora za kilimo cha zao la Pamba”. Aliongeza Mhe. Zakaria.

Kwa upande mwingine, Mhe. Zakaria ameahidi kutoa pongezi kwa wote watakaozalisha kwa kiasi kikubwa zao la Pamba Wilayani Busega. “Vijiji 5 vitakavyofanya vizuri katika uzalishaji wa zao la Pamba tutavipongeza” alisema Mhe. Zakaria.

Awali, Balozi wa zao la Pamba Kitaifa, Bw. Aggrey Mwanri amesema kilimo cha zao la Pamba kinahitaji usimamizi na kanuni za kilimo, ambazo zitamuwezesha Mkulima kuzalisha kwa tija. Bw. Mwanri amesema kanuni muhimu zikiwemo matumizi ya Mbolea, kupanda kwa kufuata nafasi zilizopendekezwa na wataalam na matumizi ya mbegu bora, ni miongoni mwa mambo muhimu katika kuongeza tija ya zao la Pamba. Aidha, Mwanri amesema kilimo cha Pamba kinaweza kubadilisha maisha ya wananchi wa Busega kiuchumi kama kutakuwa na mkakati madhubuti wa uzalishaji wenye tija.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Burilo Deya amesema tayari mikakati imewekwa ikiwa  na malengo ya kuongeza tija ya uzalishaji wa zao la Pamba ikiwemo, Maafisa Ugani kupatiwa mafunzo ya kilimo cha uzalishaji wenye tija wa zao la Pamba, mafunzo yaliyofanyika mwezi wa nne mwishoni mwaka huu katika kituo cha utafiti wa kilimo Ukiriguru kilichopo mkoani Mwanza.

Aidha, Bw. Deya ametaja mikakati mingine ikiwemo kuanzisha mashamba darasa, kuwajengea uwezo Serikali za vijiji kuhusu uzalishaji wa zao la Pamba, kuendelea kuwajengea uwezo viongozi juu ya uzalishaji wa zao la Pamba ikiwemo wawakilishi wa wananchi na kuendelea kushirikiana kwa ukaribu na Wataalam na Bodi ya Pamba katika uzalishaji wa zao hilo. Bw. Deya ameongeza kwamba lengo la Wilaya ya Busega ni kuongeza uzalishaji kutoka wastani wa kilo 200 kwa ekari kufikia kilo 700 kwa ekari kwa msimu ujao wa kilimo.

Washiriki wa Semina hiyo ya uhamashaji wa kuongeza tija ya zao la Pamba, wamesema ni jambo muhimu sana kwa Wakulima wa zao hilo Wilayani Busega kupata elimu ya uzalishaji wa zao la Pamba, ambayo itawasaidia kuongeza tija katika uzalishaji, hivyo watakwenda kuwa mabalozi wa kilimo cha Pamba. Lengo la Wilaya ya Busega ni kuzalisha tani 50,000, huku lengo la mkoa wa Simiyu ni kuzalisha tani 500,000. Wilaya ya Busega inaendelea na kampeni ya kuongeza tija ya uzalishaji wa kilimo cha zao la Pamba katika ngazi ya vijiji, ambapo mpaka sasa vijiji vipatavyo 23 vimepatiwa mafunzo.

MWANZO.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa