• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA YA BUSEGA AELEZA MAKUBWA YALIYOFANYWA NA SERIKALI YA AWAMU YA TANO WILAYANI HUMO

Posted on: August 26th, 2020

Katika kipindi cha miaka mitano (5) chini ya Serikali ya Awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Dr. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tumeshuhudia mengi makubwa yamefanyika katika Wilaya yetu ya Busega ukilinganisha na hapo awali. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Tano Mwera wakati akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake mapema wiki hii.

Akiongea kwa ujumla Mhe. Mwera amesema awamu ya tano imefanya mambo mengi katika nchi yetu kwa ujumla, hiyo imechangiwa na uadilifu wa viongozi wengi wa serikali ya awamu hii ya tano. Mapambano dhidi ya rushwa iliyokithiri, kuimarika kwa ukusanyaji mapato, elimu bila malipo, ujenzi wa miundombinu ya barabara, uwajibikaji wa watumishi ni miongoni mwa mambo makubwa yaliyosimamiwa vyema na Mhe. Magufuli, aliongeza Mhe. Mwera.

Wilaya ya Busega imeweza kutekeleza miradi mingi chini ya serikali ya awamu ya tano katika kipindi cha miaka mitano. Ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya wilaya ya Busega ambalo linagharimu TZS Bilioni 4.9 ambapo mradi umefikia asilimia 60%. Sambamba na ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri, pia serikali imeweza kujenga jengo la Ofisi ya Mkkuu wa Wilaya ambapo gharama yake ni TZS Bilioni 1.1 na mpaka sasa limefikia asilimia 98%.

Kwa upande wa Afya, ujenzi wa Hospitali ya Wilaya umegharimu TZS Bilioni 1.8 na huduma zimeanza kutolewa huku baadhi ya miundombinu ikiendelea na ujenzi wake. Licha ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya, pia upanuzi wa vituo vya Afya ili kuboresha huduma za afya Wilayani Busega umetekelezwa na serikali.

Upanuzi wa Vituo vya Afya vya Nassa na Igalukilo kwa TZS. 850 Milioni. Pia serikali kwa kushirikiana na wadau wa afya imeweza kuboresha miundombinu kwenye vituo vya afya na zahanati kwa gharama ya TZS. Milioni 606.5 katika zahanati za nyamikoma, Mwasamba, Mwanhale, Ijiha, Nyaluhande, Mwamagigisi, badugu, Ngasamo, Kalemela na vituo vya afya vya Kiloleli na Lukungu.

Aidha Mhe. Mwera amesema mapinduzi makubwa yamefanyika Wilayani Busega kwa upande wa elimu mpaka sasa tumepataTZS Bilioni 2.7 kwaajili ya elimu bila malipo wilayani Busega. Hali hii imefanya ufaulu kupanda kwa upande wa shule za msingi kutoka asilimia 73.8% mwaka 2015 mpaka asimilia 90.2% mwaka 2019. Aidha Mhe. Mwera amekiri kupanda kwa ufaulu kwa shule za sekondari kutoka asimilia 58% mwaka 2015 mpaka kufikia asilimia 77% mwaka 2019.

“kwa upande wa elimu tumepanda sana na kwa mwaka jana tumeweza kuingiza wanafunzi wanne kitaifa kwa matokeo ya mtihani wa darasa la saba, sio kitu kidogo kwa wilaya yetu kuingiza watoto wanne kwenye wanafunzi 10 bora kitaifa, kwa hilo tunajivunia sana”, aliongeza Mhe. Mwera.

Pamoja na kuimarika kwa elimu wilayani Busega, pia serikali imeweza kujenga miundombinu ya elimu ili kuchochea upatikanaji wa elimu bora ikiwemo ujenzi wa shule tatu (3) mpya za sekondari katika kipindi cha miaka mitano chini ya serikali ya awamu ya tano. Ujenzi wa shule ya Sekondari ya Dr. Chegeni, shule ya Sekondari Masanza na Shule ya sekondari Antony Mtaka imesaidia kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaojiunga kidato cha kwanza na kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani. Ujenzi wa shule hizo mpya 3 za sekondari kumeifanya wilaya kuwa idadi ya shule za sekondari zipatazo 20.

Kwa upande wa miundombinu ya barabara, serikali imeweza kuboresha na kuongeza mitandao ya barabara wilayani Busega kutoka barabara 36 zenye urefu wa kilomita 326.99 mwaka 2015 mpaka barabara 136 zenye urefu wa kilomita 511.11 mwaka 2020.

Kuanzia mwaka 2015 serikali imeweza kutoa jumla ya fedha zaidi ya TZS Bilioni 4.689 ambapo kati ya hizo zaidi ya TZS 2.39 ni fedha za matengenezo kutoka bodi ya mfuko wa barabara na zaidi ya TZS 2.29 ni fedha za miradi ya maendeleo (MIVARF).

Miundombinu ya maji imetekelezwa kwa ukubwa kwa kipindi cha miaka mitano ikiwemo utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Lamadi wenye thamani ya TZS Bilioni 12.8 ambao umekamilika na tayari unatumika.

Miradi mingine ni pamoja na mradi wa maji Lukungu, mradi wa maji kiloleli, mradi wa maji Badugu, mradi wa maji Nyashimo, mradi wa maji Bushigwamhala na mradi wa maji Busami na jumla ya gharama ya miradi hiyo tajwa kwa ujumla katika kipindi cha miaka 5 kuwa na thamani ya Zaidi ya TZS Bilioni 5.7.

Nishati katika Wilaya ya Busega imekuwa ya kuridhisha huku Mhe. Mwera akiishukuru serikali kwa kunufaika sana na mpango wa usambazaji umeme vijijini (REA). Kutoka mwaka 2015 ni vijiji 24 viliunganishwa na huduma ya umeme kati ya vijiji 59 lakini mpaka kufikia 2020 takribani vijiji 53 vimeunganishwa na huduma ya umeme, hivyo ni vijiji 6 pekee vimesalia kuunganishwa umeme, aliongeza Mhe. Mwera.

Utekelezaji wa uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya masikini (TASAF) ni miongoni mwa juhudi za serikali kuhakikisha wananchi wanakua kiuchumi kwa kuongeza kipato.

Wilaya ya Busega imeweza kuwezesha wananchi kwa kupitia vikundi vya Wanawake, Vijana na Walemavu kwa kuwapatia mikopo ya masharti nafuu, huku zaidi ya TZS milioni 188, vikundi vya Wanawake kutoka 26 mwaka 2015/2016 kufikia vikundi 51 mwaka 2019/2020 hivyo kufanya thamani ya mikopo kuwa zaidi ya TZS milioni 86.2, vikundi vya Vijana kutoka 13 mwaka 2015 hadi 23 mwaka 2019/2020 na thamani ya mikopo kuwa zaidi ya TZS milioni 71.6. Halikadhalika utoaji mikopo kwa vikundi vya watu wenye ulemavu umeongezeka kutoka kikundi 1 mwaka 2015/2016 hadi kufikia vikundi 7 mwaka 2019/2020 na kufanya gharama za mikopo kufikia zaidi ya TZS milioni 19.5.

Mpango wa kunusuru kaya masikini, TASAF umeweza kutekelezwa vyema wilayani Busega kwani kuanzia mwaka 2015/2016 mpaka 2019/2020 jumla ya kaya 4180 zimeweza kunufaika na mpango huo ambapo jumla ya TZS Bilioni 3.744 zimetumika.

Serikali imefanya mambo mengi wilayani Busega na kwakweli ni jambo la kumshukuru sana Mhe. Dr. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutupendelea sana katika kipindi hiki cha miaka mitano chini ya serikali ya awamu ya tano kwani Busega ya miaka mitano nyuma sio hii ya sasa, alisema Mhe. Mwera.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa