• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Miradi Saba ya Maendeleo Busega Yakaguliwa na Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu; Kwa Kiasi Kikubwa Yaridhishwa na Utekelezaji Wake

Posted on: August 17th, 2021

Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu imeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo Wilayani Busega katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021. Kamati hiyo imefanya ziara ya siku moja Wilayani Busega siku ya tarehe 16 Agosti 2021.

Katika ziara hiyo wajumbe wa Kamati hiyo wakiongozwa  na Mjumbe Halmashauri Kuu Taifa Mkoa wa Simiyu Bw. Emmanuel Silanga imeweza kutembelea Miradi ipatayo 7. Bw. Silanga amesema kwa kiasi kikubwa kamati hiyo imeridhishwa na Utekelezaji wa Miradi ambayo imetembelewa.

Aidha, Kamati hiyo imetaka ushirikishwaji wa Utekelezaji wa Miradi mbalimbali kwa Wananchi,  na Viongozi ikiwemo Madiwani na Wenyeviti wa Vijiji. Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Simiyu Bw. Mayunga George amesema kumekuwa na malalamiko makubwa kwa Wananchi na Viongozi kuhusu kutoshirikishwa Utekelezaji kwa baadhi ya Miradi.

Kwa upande mwingine Bw. Silanga amesema pamoja na kuridhishwa na kazi nzuri ya Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo Wilayani Busega, lakini ni muhimu Miradi hiyo kukamilika kwa wakati ili kuondoa changamoto mbalimbali ambazo ni kero kwa Wananchi. Bw. Silanga ameendelea kwa kusema kwamba Wakanadarasi wengi wamekuwa wakichelewesha Miradi mingi hivyo mamlaka husika zisimamie vyema ili Miradi ikamilike kwa wakati uliopangwa.

Pamoja na hayo, wajumbe wa kamati hiyo wameshauri kwamba ni muhimu taarifa za Fedha za Miradi husika ziwe wazi kwa Wananchi. Aidha, kwa upande mwingine wamemuomba Meneja wa Wakala wa barabara vijijini na mijini (TARURA) Wilaya ya Busega kuwasimamia vyema Wakandarasi wanaoingia nao mikataba ya ujenzi wa Barabara zinazojengwa kuwa na ubora ili ziweze kudumu kwa muda mrefu.  

Nae, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amesema uongozi wa Wilaya utafanyia kazi maeneo yote yanayoonekana kuwa na changamoto na kuiahidi Kamati hiyo kwamba mapungufu yote yatafanyiwa kazi. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Busega Bi. Veronica Sayore amesema kwamba ana imani kubwa ya kuendelea kutekeleza Miradi ya Maendeleo na kwamba maelekezo yote yaliyotolewa na Kamati hiyo ili kufikia malengo ya Serikali katika kutekeleza Miradi ya Maendeleo.

Miradi iliyotembelewa na kamati hiyo ni mradi wa ujenzi wa Zahanati ya imalamate ambayo mpaka sasa umegharimu zaidi ya Tshs Milioni 48, ujenzi kilomita 22 barabara ya Busami-Mwanangi na Bombabija-Kajila Katekista kwa thamani ya zaidi  Tshs Milioni 100, mradi wa ujenzi wa wodi 3 Hospitali ya Wilaya; Wodi ya Wanaume, Wanawake na Watoto kwa thamani ya Tshs Milioni 500, mradi wa miundombinu ya Madarasa na Maabara katika Shule mpya ya Sekondari Venance Mabeyo ambapo mpaka sasa thamani iliyotumika ni zaidi ya Tshs Milioni 92, ujenzi wa Madarasa Shule ya Msingi Mwabasabi kwa thamani zaidi ya ya Tshs Milioni  72.8, na mradi wa ujenzi wa tanki la maji Kata ya Mkula kwa thamani ya Tshs Bilioni 2.1.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa