• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MHE. MKUU WA MKOA WA SIMIYU, ANTONY MTAKA AAGIZA KUFUATWA KWA TARATIBU ZA MALEZI YA WATOTO WENYE ULEMAVU WA NGOZI

Posted on: February 4th, 2020

Kituo cha kulea watoto wenye ulemavu wa ngozi kilichopo kata ya Lamadi Wilayani Busega kimetakiwa kufuata taratibu za malezi ya watoto wenye mahitaji maalum. Kituo cha Bikira Maria Mama wa Mungu kina jumla ya watoto wapatao 70. Mkuu wa mkoa ametoa maagizo hayo, licha ya awali kituo hicho kupewa  taratibu za uendeshaji wake kutoka ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega.

Mhe. Antony Mtaka amefika kituoni hapo na kusikia changamoto na sintofahamu ya uendeshaji wa kituo hicho ambacho hapo awali kilionekana kina malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi waishio karibu na maeneo hayo na kupelekea uongozi wa Wilaya kutembelea kituo hicho na kugundua baadhi ya changamoto ikiwemo kujiendesha bila ya kusajiliwa pia kutokuwa na wataalam wa ustawi wa jamii kwenye kituo hicho.

Kabla ya ziara ya Mkuu wa Mkoa kituoani hapo, kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya ya Busega ilitoa maelekezo kituoni hapo jinsi ya taratibu za malezi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi (albino) na utambuzi kwa kufanya usajili. Kwenye ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Busega Mh. Tano Mwera alisisitiza ubora wa malezi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi uendane na uhalisia wa maisha yao ya kila siku. Aliyasema hayo alipotembelea kituoni hapo tarehe 31 Januari 2020 na kusisitiza kituo hicho kisingetambulika kama kisingefata taratibu za uendeshaji na sifa za malezi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi.  

Kwa upande mwingine ziara ya Mkuu wa Mkoa kwenye kituo hicho ni msisitizo wa uendeshaji wa kituo hicho kwa utaratibu ambao unakidhi haja ya kuwepo kwa malezi bora kwa watoto wenye mahitaji maalum. “Kituo kina muonekano wa mazingira mazuri lakini kimekosa baadhi ya sifa za utendaji na utaratibu wa malezi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi ndio sababu kubwa ya kufanya ziara ya kukitembelea ili kujiridhisha na baadhi ya malalamiko yanayojitokeza kuhusu kituo hicho” alisisitiza Mhe. Antony Mtaka.

Mbali ya ziara ya awali ya Mkuu wa Wilaya ya Busega, pia Mkuu wa Mkoa ameagiza kuwepo kwa ukaribu baina ya Mlezi wa watoto wa kituo hicho na uongozi mzima wa Wilaya ya Busega, kwani uwepo wa kituo hicho ni msaada mkubwa kwa watoto hao. Amemsisitiza Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoani na Wilaya ya Busega washirikiane na mlezi wa watoto wa kituo hicho ili kuhakikisha kituo hicho kinakidhi hadhi ya kulea watoto, ikiwemo kufanya taratibu za usajili, kushirikiana na mlezi wa watoto wa kituo hicho katika kulinda afya na malezi bora ya watoto hao.

Kwa upande mwingine mlezi wa watoto kituoni hapo, Sister Hellena Ntambulwa ameshukuru uongozi wa serikali ngazi ya Mkoa na Wilaya kwa kutembelea kituo hicho na ameahidi kushirikiana na uongozi wa serikali ya Wilaya kuhakikisha taratibu za usajili na uendeshaji wa kituo hicho zinakamilika. Hata hivyo mlezi huyo amekiri kutokuwa na ufahamu wa kutosha kwa baadhi ya mambo machache juu ya uendeshaji wa malezi ya watoto hivyo ameahidi kufuata taratibu zinazotakiwa na pia kushirikiana na uongozi wa serikali ya Wilaya kwa lengo la kukidhi mahitaji ya malezi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi.

Kituo cha Bikira Maria Mama wa Mungu kilianzishwa mwaka 2011 na kugundulika kufanya kazi kwa kutofata baadhi ya taratibu licha ya kutakiwa kufuata taratibu kwa kupewa maelekezo mara kwa mara kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega jinsi ya kuendesha kituo hicho, lakini bado hakukuwa na mafanikio, hivyo kupelekea Mkuu wa Wilaya kufanya ziara mapema mwezi uliopita tarehe 31 Januari na baadae leo tarehe 4 Februari, Mkuu wa Mkoa Mhe. Antony Mtaka, amefanya ziara ya kujiridhisaha na hali ya sintofahamu ya kituo hicho na kuagiza kufuatwa kwa utaratibu wa uendeshaji malezi ya watoto wenye mahitaji maalum kwenye kituo hicho.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa