• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru 2021 Wilayani Busega

Posted on: June 29th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria, viongozi wengine waWilaya, kwa kushirikiana na Watumishi pamoja na  Wananchi wa Busega wameupokea Mwenge wa Uhuru, tarehe 28 Juni 2021. Awali, akiupokea Mwenge wa Uhuru, mapokezi yaliyofanyika katika Kijiji cha Lukungu, Kata ya Lamadi, Mkuu wa Mkoawa Simiyu, Mhe. David Kafulila kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Ali Hapi,amesema Mkoa wa Simiyu upo tayari kukimbiza Mwenge wa Uhuru katika Wilaya zotetano. Wilaya ya Busega imeupokea Mwenge wa Uhuru kutoka Wilaya ya Bunda Mkoa wa Mara.

Salamu za Awali za Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru 2021 

Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru 2021, Luteni Josephine Paul Mwambashi, ameweza kutoa salamu na ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa wakazi wa Busega. Luteni Mwambashi amesisitiza masuala muhimu ikiwemo matumizi ya malipo ya kietroniki katika ukusanyaji wa mapato kwa ngazi ya Halmashauri, kudhibiti madawa ya kulevya, lishe bora ili kujenga jamii imara na kuendelea kupima maambukizi ya virusi vya Ukimwi  ili kuikinga jamii yetu. Luteni Mwambashi amesisitiza matumizi ya TEHAMA katika kuchochea maendeleo kama kauli mbiu ya Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru 2021, inavyosema "TEHAMA ni Msingi wa Taifa Endelevu, Itumike kwa Usahihi na Uwajibikaji".

Yaliyojiri Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru 2021 Wilayani Busega

Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru zimepokelewa siku ya tarehe 28 Juni 2021 na kupita katika miradi sita kwaajili ya kuzindua, kuweka jiwe la msingi na kutembelea. Akiupokea Mwenge wa Uhuru, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amesema Wilaya yake imejipanga kikamilifu kuupokea na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru katika miradi yote iliyopangwa.

Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru 2021 Luteni Josephine Paul Mwambashi amewapongeza Wananchi wa Wilaya ya Busega kwa kushiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo. “Nawapongeza wananchi kwa kushiriki katika utekelezaji wa miradi mbalimbali, Serikali inatekeleza fedha nyingi za miradi lakini Wananchi mkishiriki kikamilifu katika miradi hiyo lazima tuwapongeze, alisema Luteni Mwambashi.

 

Aidha, Luteni Mwambashi amesisitiza utunzaji wa nyaraka za miradi mbalimbali ili kuonesha uhalisia wa utekelezaji wa miradi hiyo. Amesema ni vyema nyaraka na vilelezo muhimu viambatane na taarifa za miradi. Aidha, Luteni Mwambashi ameweza kutembelea banda la Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, TEHAMA na kupata maelezo ya baadhi ya mifumo ikiwemo mfumo wa ukusanyaji Mapato ya Serikali na mingineyo. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amewashukuru viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Busega kwa kuonesha mshikamano katika mapokezi na ushiriki wao katika Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru.

Miradi ipatayo sita imeweza kupitiwa na Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru 2021 Wilayani Busega kwaajili ya kuzinduliwa, kuwekwa jiwe la msingi na kutembelewa. Miradi hiyo imejumuisha mradi wa Ujenzi Zahanati ya kijiji cha Mkula wenye thamani ya TZS Milioni 104.3, mradi wa ujenzi wa Hotel ya Sandmark wenye thamani ya TZS Bilioni 2.2, mradi wa Maji Nyashimo wenye thamani ya TZS Bilioni 2.287, Club ya Wapinga Rushwa ambapo mpaka sasa thamani yake TZS 80,000, mradi wa Maabara Sekondari ya Antony Mtaka wenye thamani ya TZS Milioni 58.51 na kutembelea mradi wa kisima cha maji ambao ulizinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 ili kuangalia maendeleo ya mradi, ambao thamani yake ni TZS Milioni 16.6. Mkuu wa Wilaya ya Busega amekabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi leo tarehe 29 Juni 2021, kwaajili ya kuendelea na mbio hizo katika Wilaya zingine za Mkoa wa Simiyu.

MWISHO

Kuona Picha Zaidi Bofya Kiunganishi cha Bluu: https://web.facebook.com/Halmashauri-ya-Wilaya-ya-Busega-110384587066130

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa