• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Madiwani Busega Wataka Usimamizi Bora wa Fedha za Miradi Zitokanazo na Mapato ya Ndani

Posted on: August 27th, 2021

Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega wametaka kuwepo kwa usimamizi bora wa Fedha za Miardi zinazotokana na Mapato ya Ndani. Madiwani hao wameyasema hayo wakati wa kikao cha Baraza la kufunga Mwaka kwaajili ya kupokea Taarifa ya Utendaji na Uwajibikaji wa Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 lililofanyika leo tarehe 27 Agosti 2021.

Awali Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mhe. Sundi Muniwe amesema ni vyema kuhakikisha fedha zinazoletwa na Serikali na zile zinazotokana na mapato ya ndani zinatumika kwa wakati ili kutekeleza miradi mbalimbali kwa wakati. Aidha, Mhe. Muniwe ameongeza kwamba usimamizi bora wa fedha za miradi unaenda sambamba na uchapaji kazi wa Watumishi.

Wajumbe wa Baraza hilo wamesema kwamba wanatamani kuendelea kuona Miradi ya Maendeleo inakamilika kwa wakati ili kupunguza adha ya Wananchi kupata huduma. Aidha, Madiwani wamsema kwamba iwapo Asilimia 40 ya makusanyo ya ndani itapelekwa kwa wakati katika Miradi ikiwemo ya Ujenzi wa Madarasa na Zahanati itasaidia kuondoa changamoto kwa wananchi katika baadhi ya maeneo yenye changamoto.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bi. Veronica Sayore amesema katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2021/2022, tayari bajeti imetengwa kumalizia Miradi ya Maendeleo iliyoanza kutekelezwa. Bi. Sayore ameongeza kwamba tayari kuna juhudi za kuongeza makusanyo ya ndani ili kupata fedha za kutosha zitakazopelekwa kutumika kutekeleza Miradi ya Maendeleo.

Pamoja na hayo, Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega wameweza kuipokea taarifa hiyo ya Utendaji na Uwajibikaji wa Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021. Miongoni mwa mambo mengine yaliyoibuka katika Baraza hilo ni pamoja na asiimia 10 ya mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa makundi ya Wanawake, Vijana na Walemavu, huku Madiwani wakihoji juu ya uchelewaji wa urejeshwaji wa fedha kutoka kwa wanaofadikia na Mikopo hiyo.

Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Busega Bw. Dismas Ijagala amesema kuna ongezeko kubwa la urejeshwaji wa fedha zilizokopeshwa na hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa kwa wote ambao hawarejeshi fedha hizo kwa wakati ikiwemo kuwafikisha katika mamlaka husika ikiwemo Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao. Baraza hilo la kufunga mwaka limefanyika ikiwa ni ishara ya kuanza Mwaka mpya wa Fedha 2021/2022.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa