• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Katibu Tawala Busega Akutana na Watumishi Kusikiliza Changamoto Zao

Posted on: February 7th, 2021

Katibu Tawala Wilaya ya Busega Bw. Rutagumirwa Rutalemwa ameweza kukutana na kuongea na watumishi umma kwa lengo kuu la kusikiliza changamoto na kero zinazowakabili katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Katika ziara ya siku mbili mapema wiki iliyopita Bw. Rutalemwa alipata nafasi ya kukutana na kuongea na watumishi wa kata nne, ambazo ni kata za Lamadi, Kalemela, Mkula na Lutubiga, Bw. Rutalemwa amesema kwamba anajua kwamba katika utekelezaji wa majukumu kama watumishi wa umma changamoto haziwezi kukosekana lakini bila kuonana na watumishi ni vigumu kufanya utatuzi wa changamoto hizo.

Bw. Rutalemwa amesema ni muhimu kusiliza hoja mbalimbali za watumishi pia ni fursa nzuri ya kukumbushana haki na wajibu wa watumishi wa umma. Kwa upande mwingine Bw. Rutalemwa ametoa pongezi kwa watumishi wote wilayani Busega. “Nawapongeza sana kwani mnafanya kazi kwa kujitoa na kwa moyo wa uzalendo, hivyo ningeomba tuendelee kujitoa ili kutimiza azma ya Serikali ya kutoa huduma kwa wananchi”, aliongeza Bw. Rutalemwa.

Katika ziara hiyo Bw. Rutalemwa aliambata na baadhi ya wakuu wa Idara kutoka Ofisi ya Mkurugrnzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, akiwemo Wakuu wa Idara ya Elimu Msingi na Sekondari, Mganga Mkuu wa Wilaya, mwakilishi kutoka Idara ya Utumishi, na Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Wilaya ya Busega. Aidha watumishi wameweza kutoa baadhi ya changamoto zao zikiwemo changamoto ya uchache wa vifaa vya kutendea kazi, madai ya stahiki zao, na ubovu wa miundombinu kwa baadhi ya maeneo ya vituo vya kazi.

Hata hivyo Bw. Rutalemwa ameweza kuwatoa hofu watumishi, kwamba changamoto hizo zitatatuliwa kwani hata hapo nyuma kulikuwa na changamoto nyingi za watumishi lakini Serikali kwa kuona changamoto hizo imeweza kutatua na mpaka sasa sehemu ya changamoto hizo hazipo tena. Kwa upande mwingine amewataka watumishi wasisite kuwasilisha changamoto zao, kwani Ofisi yake ipo wazi muda wowote. Pia amewaomba watumishi kufanya kazi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa na serikali ili kufikia malengo.

Aidha, mwakilishi wa Afisa Utumishi Wilaya ya Busega Bw. Ramadhan Boimanda amewataka watumishi kufuata taratibu za utumishi, ameongea hayo alipokuwa akijibu hoja ya mtumishi aliyetaka kujua ni kwanini hakuna utaratibu wa kuwakilishwa katika uchukuaji na upelekaji wa nyaraka mbalimbali katika Ofisi ya Mkurugenzi ili kuokoa muda na kupunguza gharama. “Tunapenda mtumishi afike ofisini yeye mwenyewe ili kujiridhisha na taarifa zake na sio kumtuma mwakilishi kwani baadhi ya taarifa muhimu hatutaweza kuzipata kwa wakati, hivyo ni vyema mtumishi akafika yeye mwenyewe na nyaraka zake ili tujiridhishe”, aliongeza Bw. Boimanda.

Kwa upande mwingine Bw. Rutalemwa amewataka watumishi kutojiingiza katika masuala yatakayowafanya kupoteza sifa za utumishi ikiwemo kuijiinga katika mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi, kwani hiyo inachafua utumishi wa umma, na kuwataka wao wawe mabalozi wa mapambano ya kuzuia mimba kwa Wanafunzi.

Aidha Bw. Rutalemwa amesema utaratibu wa kukutana na watumishi ni endelevu, hivyo ataendelea kuwatembelea watumishi mara kwa mara, kwani ni imani kwamba utaratibu huo una manufaa makubwa kwa watumishi wa umma wilayani Busega.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa