• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kamati za kudumu Zatembelea Miradi ya Maendeleo Busega

Posted on: January 21st, 2021

Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira na kamati ya Elimu, Afya na Maji wilayani Busega zimetembelea miradi iliyokamilika na inayoendelea kutekelezwa wilayani Busega. Kamati hizo zilifanya ziara ya kuangalia utekelezaji miradi maendeleo mbalimbali kati ya tarehe 19 na 20 Januari, 2021. Miradi iliyotembelewa ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Stendi ya mabasi ya Wilaya ya Busega, ujenzi wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa Bwalo katika Shule ya Sekondari Antony Mtaka.

Mradi wa ujenzi wa Stendi ya mabasi inayoendelea kujengwa wilayani Busega unatarajia kugharimu TZS milioni 47 mpaka kukamilika kwake. Hayo yamesemwa na Mhandisi wa ujenzi wa Wilaya ya Busega Bw. Paul Tumbu wakati wa ziara ya kamati ya uchumi, ujenzi na mazingira ilipotembelea mradi wa ujenzi wa stendi hiyo. Ujenzi unaoendelea katika mradi wa stendi hiyo ni ukamilishaji wa choo cha abiria, eneo na kusimama magari na eneo la wafanya biashara ndogondogo.


  1.  Picha: Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira ikiwa katika eneo la Stendi ya Wilaya ya Busega ambayo inaendelea na Ujenzi.  

Stendi ya mabasi ya Wilaya ya busega inajengwa huku ikiwa ni muendelezo wa mikakati ya kuboresha huduma za usafiri wilayani Busega, huku ikiwa ni muda mrefu Wilaya kutokuwa na Stendi, hali ambayo ilikuwa ni changamoto kwa wasafiri. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Anderson Kabuko ameeleza kwamba stendi hiyo inajengwa huku ikiwa na mgawanyo wa maeneo ambapo pia imejumuisha eneo la wafanyabiashara ndogo ndogo ili na wao waweze kupata fursa ya kufanya shughuli za kibiashara katika stendi hiyo pale tu itakapoanza kutumika rasmi.Picha: Sehemu ya eneo la Stendi ya Wilaya ya Busega, Mkandarasi akiendelea na Ujenzi.  


Kwa upande mwingine, kamati ya Elimu, Afya na Maji imeweza kutembelea miradi ya ujenzi wa miundombinu katika Shule ya Skeondari Antony Mtaka na kuweza kuijonea miundombinu iliyokamilika na inayoendelea kutekelezwa. Moja ya changamoto zilizopo katika Shule hiyo ni pamoja na upungufu wa madarasa ambapo shule kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 1,578 huku ikiwa na madarasa 20, lakini uhitaji wa madarasa ukiwa ni madarasa 31.

 

Picha: Kamati ya Elimu, Afya na Maji ikiwa katika Shule ya Sekondari Antony Mtaka kuangalia miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu katika Shule hiyo.

 

Hata hivyo ujenzi wa miundombinu ikiwemo vyumba vya madarasa unaendelea na jumla ya madarasa 4 yamefikia hatua ya boma ambapo ujenzi unaendelea. “Sababu tuna upungufu wa madarasa, Wanafunzi wataanza kusomea katika Bwalo huku tukiendelea na umaliziaji wa vyumba vingine vya madarasa” alisema Kabuko. Hata hivyo shule hiyo imeweza kupokea zaidi ya TZS Milioni 196 kutoka Serikalini ambapo fedha hizo zimetumika kutekeleza mradi wa bwalo la chakula 1, vyumba 2 vya madarasa ambavyo vimekamilika na vimeanza kutumika, Ujenzi wa Maabara, na ujenzi wa matundu ya vyoo.

 

Picha: Muonekano wa Bwalo la Chakula linaloendelea na ujenzi katika Shule ya Sekondari Antony Mtaka. 

Miradi ya maendeleo ambayo inaendelea kutekelezwa wilayani Busega ni miongoni mwa mikakati ya serikali kuhakikisha huduma mbalimbali zinaboreshwa na kusogezwa karibu zaidi na wananchi. Baadhi ya wananchi wamekiri kwamba miradi iliyokamilika na inayoendelea kutekelezwa ni msaada mkubwa sana hasa kwa wananchi wenye kipato cha chini, lakini wameomba miradi mbalimbali ya maendeleo itekelezwe kwa wakati.

 

Picha: Muonekano wa madarasa 2 yaliyokamilika na tayari yameanza kutumika katika Shule ya Sekondari Antony Mtaka, ambayo yamejengwa kwa mradi wa P4R.

 


 









Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa