• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya Ushauri Wilaya ya Busega (DCC) yapitia na kushauri Rasimu ya Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2021/2022

Posted on: February 10th, 2021

Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Busega (DCC) imepitia na kushauri rasimu ya bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Busega ya mwaka wa fedha 2021/2022. Kikao cha kamati hiyo kimefanyika tarehe 9 Februari 2021 katika ukumbi wa Silisos.

Akiongoza kikao hicho Mwenyekiti wa kamati hiyo ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe.Tano Mwera, amewaomba wajumbe kutoa ushauri na mapendekezo kuhusu bajeti hiyo. Pia amewaomba wajumbe kushauri na kutoa mapendekezo ambayo wanaamini yataleta matokeo chanya ya maendeleo wilayani Busega.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Anderson Kabuko amesema, tayari upo mkakati wa kuboresha usimamizi wa vyanzo vya mapato mkakati ambao utaongeza makusanyo kutoka vyanzo vya ndani. “Tumeanza na mkakati wa kuboresha baadhi ya Idara zetu, ambapo tumeanza na Idara za Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika, Idara ya Mifugo na uvuvi na Idara ya Ardhi na Maliasili kwa kuongeza vitendea kazi ili kuwezesha upatikanaji zaidi wa makusanyo ya mapato”, Aliongeza Kabuko.

Pamoja na mambo mengine Bajeti hiyo imejikita katika kuleta matokeo chanya na yenye kugusa maisha ya Wananchi mmoja mmoja. Uandaaji wa Bajeti hiyo umejikita katika miongozo na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa malengo endelevu wa maendeleo wa mwaka 2030, dira ya taifa ya 2025, na mpango mkakati wa Halmashauri. Pia imezingatia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati wa uzinduzi wa Bunge Mwezi Novemba, 2020. Mapendekezo ya makisio ya Bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Busega kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 ni TZS Bilioni 35,175,907,278.

Vipaumbele 17 Vifuatavyo Vimeainishwa katika Rasimu hiyo:

  • Kuchangia miradi ya maendeleo kwa shughuli zinazoanzishwa na wananchi kama njia mojawapo ya kuunga mkono juhudi zao.

  • Kulipa posho za vikao na stahiki za Waheshimiwa Madiwani za kila mwezi.

  • Ujenzi wa miundombinu ya Shule za Msingi na Sekondari.

  • Kuendeleza shughuli mbalimbali za Ardhi wilayani.

  • Kugharamia zoezi la usimamizi na ukusanyaji wa mapato ya vyanzo vya ndani na kukusanya takwimu kwa kila chanzo.

  • Kugharamia ujenzi wa masoko ya Masanza, Mwamagigisi, na Nyashimo.

  • Kuendeleza ujenzi wa stendi ya Nyashimo.

  • Kuboreha huduma za uvuvi.

  • Kuhamasisha ufugaji bora na kutoa chanjo za mifugo.

  • Kuongeza vitendea kazi kama vile pikipiki na magari.

  • Kuboresha huduma za Afya.

  • Kugharamia uendeshaji wa Ofisi na vikao mbalimbali vya kisheria.

  • Kujenga vizimba vya kufugia Samaki ili kujiongezea mapato.

  • Kuendeleza shughuli za ugani kama kilimo cha mazao ya biashara na chakula na mifugo kwa kuhamasisha wananchi kupanda mbegu bora za Pamba na kuanzisha mashamba darasa ya mazao ya Pamba na Alizeti.

  • Kutoa mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali, Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu.

  • Kuboresha usafi wa mazingira.

  • Kugharamia malipo ya vibarua.

Aidha wajumbe wa kikao hicho walipata fursa ya kushauri maeneo mbalimbali ya Rasimu ya Bajeti. Kikao hicho kilihudhuriwa na wajumbe kutoka Vyama vya Siasa, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Wakuu wa Idara na Vitengo, Watendaji wa Kata, wawakilishi kutoka Sekta binafsi, Wadau wa Maendeleo, Viongozi wa Dini, na wawakilishi kutoka Taasisi zisizo za Serikali.

Kwa upande mwingine, kamati hiyo imepitia na kushauri Mapendekezo ya Bajeti za taasisi zingine za Kiserikali zilizopo wilayani Busega, ambazo ni Bajeti ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA).

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa