• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kafulila: Serikali kuanzisha Chuo cha Kilimo na Mifugo Mkoani Simiyu

Posted on: January 28th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila amesema Serikali imedhamilia kuanzisha chuo cha Kilimo na Mifugo Mkoani Simiyu. Kafulila amesema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Itwimila B Kata ya Kiloleli Wilayani Busega. Katika kikao hicho cha hadhara wakazi wa Kata hiyo miongoni mwa mambo mengine walitaka kujua mpango wa Serikali kuhusu uwepo wa chuo katika mkoa wa Simiyu.

Kafulila amesema Serikali imedhamilia kujenga chuo hicho ili kuongeza tija kwa vijana kupata maarifa katika masuala ya kilimo na mifugo. “Hiyo ni fursa kwa vijana wetu wa mkoa wa Simiyu, kwani watapata maarifa na ujuzi kupitia chuo hicho kitakachojengwa Malampaka wilayani Maswa” alisema Kafulila.

“Majengo yanayotumika kwa sasa katika ujenzi wa reli kisasa (SGR) maeneo ya Malampaka baada ya kukamilika mradi huo majengo hayo yatatumika kama chuo cha Kilimo na Mifugo”, aliongeza Kafulila.

Aidha, Kafulila amesema kwamba Serikali pia imetenga fedha kwaajili ya kujenga chuo cha ufundi stadi (VETA) mkoani Simiyu na ujenzi unatarajiwa kuanza mwezi wa sita mwaka huu. Kafulila amesema hayo akijibu swali lililoulizwa na mwananchi ambalo lilitaka kujua mpango wa Serikali kuhusu chuo cha ufundi stadi katika mkoa wa Simiyu.

Katika ziara hiyo Kafulila ameweza kusikiliza changamoto na kero za wananchi, miongoni mwa kero hizo ni pamoja na uvamizi wa wanyama katika makazi ya wananchi wakiwemo viboko. Wananchi hao wamesema uvamizi wa viboko katika makazi ya wananchi na maeneo ya mashamba imekuwa ni kero kubwa maeneo tofauti katika Kata hiyo. Kafulila amewatoa hofu wakazi wa Kata hiyo kwa kuwaeleza kwamba suala hilo lipo katika utaratibu wa kuhakikisha kero hiyo inapatiwa mwarubaini wake.

Kwa upande mwingine Kafulila ameweza kutumia fursa ya kikao hicho kueleza masuala machache miongoni mwa mengi yanayotekelezwa na Serikali ya awamu ya sita. Kafulila amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza miradi yote iliyoanzishwa katika awamu ya tano ikiwemo mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), ujenzi wa daraja la Busisi-Kigongo, ujenzi wa bwawa la Mwalimu Nyerere na miradi mingineyo. Aidha, Kafulila amesema kwa kujali manufaa ya wananchi Serikali ya awamu ya sita imeweza kujenga madarasa 15,000 nchi nzima kwa shule za sekondari na shule shikizi, ambapo kwa mkoa wa Simiyu vyumba vya madarasa  449 vimeweza kujengwa.

Akitoa ufafanuzi wa huduma ya gari la maji taka, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amesema taratibu za gari hilo zinaendelea na kikubwa kwasasa ni uandaaji wa  miundombinu ili kuweka mazingira bora ya huduma hiyo. Kwa upande mwingine Kafulila ametoa ufafanuzi wa gharama za bei ya uunganishaji wa umeme huku akisisitiza kwamba maelekezo ya Serikali yanataka maneneo yote ambayo ni ya vijijini gharama ya kuunganisha umeme ni TZS 27,000. “Sehemu kubwa ya mkoa wa Simiyu ni vijijini hivyo uunganishwani wa umeme unabaki kama ilivyo awali isipokuwa maeneo ambayo ni ya miji kama ilivyo Bariadi mji na maeneo mengine machache.

Wananchi waliohudhuria kikao hicho wameipongeza Serikali kwa maono ya kuanzisha chuo cha Kilimo na Mifugo kwani vijana wengi wa ndani ya mkoa wa Simiyu na maeneo mengine ya nchini watapata fursa ya maarifa na ujuzi katika sekta ya Kilimo na Mifugo. Halikadhalika wananchi hao wameipongeza Serikali kwa hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara, shule na mahospitali.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa