• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Jumla ya TZS 2,245,850,000 kujenga barabara za Vijijini Wilayani Busega

Posted on: January 24th, 2022

Zaidi ya Bilioni 2.245 zinatarajia kutumika kujenga barabara za vijijini Wilayani Busega. Hayo yamesemwa na Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Mwita Muhochi katika kikao kilichofanyika siku ya tarehe 24/01/2022 kwaajili ya kupitia utekelezaji wa miradi ya barabara kwa mwaka 2021/2022 na kupitia mapendekezo ya mpango wa mwaka 2022/2023 kwa wadau wa barabara.

Katika kikao hicho, Mhandisi Muhochi amesema kwamba Serikali imeleta kiasi hicho ili kuhakikisha barabara za vijijini zinajengwa kwa ubora ili kuondoa changamoto za miundombinu ya barabara Wilayani Busega.

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan ina malengo makubwa ya kuhakikisha barabara zinajengwa maeneo mbalimbali kwa ubora unaotakiwa. Aidha, Zakaria amesme licha ya Serikali kuleta fedha hizo ni vyema watekelezaji kuwa na usimamizi mzuri ili ziweze kutumika kwa ufanisi mkubwa. “Niwapongeze TARURA kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya lakini ni muhimu Wakandarasi tunaowapa kazi wawe na uwezo wa kufanya kazi, kwani baadhi wamekuwa na shida ya kutokamilisha miradi ya ujenzi wa barabara kwa wakati” alisema Zakaria.

Kutowapa nafasi Wakandarasi wanaochelewesha kazi ni miongoni mwa mambo yaliyo jadiliwa kwa kina katika kikao hicho, huku wadau mbalimbali wakikiri kwamba kuna baadhi ya wakandarasi wamekuwa wakichelewesha ujenzi wa miradi ya barabara hivyo kusababisha adha kwa wananchi wa maeneo husika.

Aidha, Zakaria amewataka TARURA kushirikiana na madiwani katika miradi ya ujenzi wa barabara ili kuleta tija ya utekelezaji wa miradi hiyo katika maeneo husika. “Madiwani wakishirikishwa ipasavyo itasaidia kuleta tija na vipaumbele katika maeneo husika”, aliongeza Zakaria.

Wadau walioshiriki kikao hicho wanasema kwamba kazi kubwa imefanywa na TARURA kwani kwasasa sehemu kubwa ya Wilaya inafikika ukilinganisha na hapo awali. Aidha, wameomba barabara ambazo bado hazijasajiliwa kwenye mtandao wa barabara zisajiliwe ili ziweze kufunguliwa, na barabara zote ambazo zina umuhimu mkubwa kwa uchumi wa wananchi kupewa kipaumbele katika matengenezo. Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Mhe. Sundi Muniwe amesema kwamba madiwani wataendelea kushirikiana na TARURA ili kuhakikisha barabara zinajengwa kwa ufanisi mkubwa.

Mtandao wa barabara Wilayani Busega ni kilomita 511 huku kilometa 159.73 sawa na asilimia 31 zipo katika hali nzuri, kilometa 124.01 sawa na asilimia 25 zipo katika hali ya wastani na kilometa 227.36 sawa na asilimia 44 bado zipo katika matengenezo ya awali, wakati asilimia 35 ya barabara zilizotengenezwa zipo katika kiwango cha changarawe (moram) na asilimia 65 ni barabara za udongo. TARURA Wilaya ya Busega inatarajia kutengeneza barabara zipatazo 30 zenye urefu wa zaidi ya kilometa 68.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa