• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC Gabriel Zakaria: Tutaboresha Miundombinu ya Umeme na Barabara Mgodi wa Imalamate

Posted on: July 27th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria amesema atafanyia kazi vilio vya wachimbaji wadogo katika mgodi wa Imalamate, ambao wameomba uongozi wa Wilaya ya Busega kupeleka huduma ya nishati ya umeme na kujenga barabara itakayowezesha kuboresha mazingira ya mgodi huo, hivyo kuongeza uzalishaji. Mhe. Gabriel Zakaria ameyasema hayo tarehe 26 Julai 2021 alipotembelea mgodi huo kusikiliza kero za wachimbaji wadogo.

Katika kikao hicho, Mhe. Gabriel Zakaria ameweza kusikiliza kero zilizopo katika mgodi huo, huku akisisitiza kwamba kero zilizobainishwa zitatatuliwa kwani anapenda kuona kila mchimbaji katika mgodi huo anapata haki yake. “Mimi ni mhubiri wa amani na haki, hivyo sitopenda kuona mnakosa haki yenu kwani wote mnatafuta” aliongeza Mhe. Gabriel Zakaria.

Mhe. Gabriel Zakaria amesema amesikia vilio na kero za wachimbaji wadogo, hasa kero ya kutokuepo kwa umeme wa uhakika na miundombinu mibovu ya barabara, hivyo amesema atahakikisha huduma ya nishati ya umeme inafika katika mgodi huo. “NItaongea na na TANESCO ili kufanikisha huduma ya nishati katika mgodi huo” alisema Mhe. Gabriel Zakaria. Aidha, Mhe. Gabriel Zakaria amewatoa hofu wachimbaji wadogo, na kusema kwamba anaelewa changamoto zinazowakabili wachimbaji hao ikiwemo ya kukosa huduma ya nishati ya umeme ambayo inasababisha kuwepo kwa uzalishaji mdogo na wizi hasa nyakati za usiku.

Kero nyingine zilizobainishwa na wachimbaji hao ni pamoja na tozo na kodi kubwa, kutofanyika kwa mnada kwa wakati, na matukio ya uhalifu nyakati za usiku. Akijibu Sehemu ya kero hizo Afisa Madini Mkoa wa Simiyu Mhandisi Amini Msuya amesema kuwa mchimbaji yeyote atakayepata kero au changamoto awasilishe malalamiko katika vyombo vinavyohuskia ikiwemo Ofisi ya Madini Mkoa, na malalamiko yatafanyiwa kazi kwa wakati.

Kwa Upande miwngine Mhandisi Msuya ameweza kutoa ufafanuzi wa mgawanyo wa mifuko ya mchimbaji, akisema kwamba asilimia 70 ya mifuko ni mali ya mchimbaji, wakati asilimia 20 ni ya kampuni yenye leseni na asilimia 10 ni mali ya mwenye shamba, huku akiwataka wamiliki wa leseni kutozidisha asilimia za mgawanyo wa mifuko kwani kufanya hivyo ni kukiuka utaratibu na miongozo.

Mhe. Gabriel Zakaria kwa mara ya kwanza ametembelea mgodi wa Imalamate huku akiweka dhamira ya kutatua kero za wachimbaji wadogo, ambapo mgodi huo una zaidi ya wachimbaji wadogo 5,000.   Mhe. Gabriel Zakaria amesema iili kutengeneza mazingira bora ya kufanyia kazi, ni lazima malalamiko ya  wachimbaji wadogo yafanyiwe kazi, lakini pia kuboresha miundombinu katika mgodi huo.  

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa