• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Busega Kuongeza Thamani ya Zao la Pamba

Posted on: May 2nd, 2021

Wakulima Wilayani Busega wametakiwa kuongeza thamani ya zao la Pamba kwa kufuata njia bora za kilimo na njia bora za uchakataji pamba kwa kutumia mashine. Hayo yamesemawa na Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Anderson Kabuko wakati wa mafunzo ya kilimo cha pamba yaliyofanyika katika kituo cha utafiti wa kilimo Ukiriguru mkoani Mwanza. Katika mafunzo hayo yaliyofanyika kuanzia tarehe 26 hadi 30 Aprili, 2021 yamehusisha maafisa ugani na wadau wa kilimo kutoka Wilayani Busega.

“Tunataka kufanya mapinduzi ya kilimo cha pamba kwa kuongeza uzalishaji wa kilimo hicho Wilayani Busega, baada ya mafunzo haya tutapita katika kata zetu kutoa elimu ya uzalishaji wa kilimo cha pamba” alisema Kabuko. Katika mafunzo hayo miongoni mwa elimu muhimu waliyoipata washiriki ni pamoja na uongezaji wa thamani wa zao la pamba.

Kwa upande mwingine, Bw. Kabuko amesema licha ya dhamira ya Wilaya kuboresha uzalishaji wa zao la pamba kwa kuongeza uzalishaji, suala la thamani ni kipaumbele katika kulinda maslahi ya mkulima na hivyo halitachukua muda mrefu katika utekelezaji wake. “Ni vyema kuongeza thamani ya pamba, hivyo tunadhamiria kuanza na mashine kwa baadhi ya maeneo machache na baadae kununua mashine za kutosha” aliongeza Kabuko.

Awali, Kaimu Mkurugenzi kituo cha utafiti wa kilimo Ukiriguru Dkt. Henerico Kulembeka, amesema ili kuboresha zao la pamba ni muhimu zao hilo liwe na manufaa kwa wakulima, hivyo ni muhimu kutumia mashine katika uchakataji ili kuongeza thamani ya pamba kwa kupata pamba nyuzi, mbegu, mafuta na mashudu ambayo hutumika kama chakula cha mifugo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Busega Mhe. Sundi Muniwe, amewataka maafisa ugani kutumia elimu waliyoipata kuongeza uzalishaji wa zao la pamba ili Wilaya ya Busega iwe mfano wa kuigwa. Pia Mhe. Muniwe amesema ili kuleta ufanisi wa dhumuni la mafunzo hayo ni vyema kushirikiana na vyama vya ushirika na kuhamasisha matumizi ya mashine ya kuchakata pamba ili kutenganisha pamba nyuzi, mbegu, mafuta na mashudu kwa lengo la kuongeza thamani. “Tumekuja kujifunza, na tunaamini tumepata kitu kikubwa na tutafanya mapinduzi makubwa katika kilimo cha pamba katika Wilaya ya Busega” alisema Mhe. Muniwe.

Zao la pamba Wilayani Busega ni miongoni mwa mazao ya biashara yanayolimwa na wakulima wengi Wilayani Busega, lakini uzalishaji wake ni mdogo kwani kwa ekari 1 kwasasa huzalisha kilogramu 175 hadi 200. Hivyo, lengo la mafunzo ni kuhakikisha uzalishaji wa pamba unapanda kutoka msimu mmoja hadi mwingine. Ili kuongeza uzalishaji Bw. Kabuko amesema malengo ya Wilaya ni kuzalisha wastani wa kilogramu 1,200 kufikia mwaka 2024/2025.

Katika mafunzo hayo washiriki wameweza kupata elimu ya kanuni bora za kilimo cha pamba, njia ya kisasa ya uzalishaji wa mbegu za pamba, udhibiti wa magonjwa shambulizi kwa zao la pamba, matumizi ya bora ya mbolea elekezi na uongezaji wa thamani ya pamba. Wadau walioshiriki mafunzo hayo wamesema elimu waliyoipata ina manufaa makubwa katika kilimo cha pamba, hivyo wameomba utekelezaji ufanyike ili kupata matokeo yaliyokusudiwa. Kwa upande wao maafisa ugani, wamekiri kwamba licha ya changamoto zilizopo kweye kilimo cha pamba, lakini kwa kupitia mafunzo hayo wanaamini watafanya kile kinachokusudiwa ili kuleta mapinduzi makubwa kwenye kilimo cha pamba Wilayani Busega.

MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa