• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Baraza la Madiwani laomba TEMESA kuboresha Utengenezaji wa Magari ili kupunguza Gharama Kubwa ya Matumizi ya Fedha za Halmashauri

Posted on: April 3rd, 2020

Kikao cha baraza la madiwani robo ya pili Oktoba-Disemba 2019/2020 kimefanyika tarehe 03.04.2020, huku madiwani wakitaka upembuzi wa masuala mbalimbali ikiwemo utendaji wa wakala wa ufundi wa umeme na utengenezaji wa magari ya serikali, TEMESA na utekelezaji wa  ujenzi wa stendi ya mabasi ya wilaya ya Busega.

Katika kikao hicho kilichokuwa na wajumbe mbalimbali na madiwani kutoka kata zote 15 na wale wa viti maalum, kilikuwa na hoja na maazimio ya kuleta ufanisi wa masuala mbalimbali katika wilaya ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Busega.

Suala la matengenezo ya magari ya halmashauri ni moja kati ya jambo lililochukua nafasi kubwa miongoni mwa madiwani, ikielezwa utengenezaji wa magari ya halmashauri unagharimu fedha nyingi lakini huchukua muda mfupi kwa magari hayo kuwa na ubovu. Magari ya halmashauri hutengenezwa na TEMESA lakini huchukua muda mfupi kwa magari hayo kuwa na ubovu.

Kaimu Meneja TEMESA Mkoa wa Simiyu, Ramadhan Ally ameeleza kuwa kuna ubovu wa magari unaojitokeza baada ya kumaliza kufanyiwa matengenezo hivyo hupokea tena magari hayo kwa muda mfupi yakiwa yana ubovu mwingine. Hata hivyo baraza la madiwani limeiomba TEMESA kuwa na ufanisi wa utengenezaji wa magari ya halmsahauri huku ikiridhia kama hali haitakuwa na uboreshwaji basi wataomba kutopeleka magari ya halmashauri na kutafuta fundi mwingine kwaajili ya matengenezo ya magari ya halmashauri.

“kwakuwa inaonekana ni kama uzembe, na hilo linatugharimu sana kwa upande wa matumizi ya fedha za halmashauri na kufanya tukose pesa kwa ajili ya shughuli zingine muhimu, hivyo tunaomba TEMESA waboreshe utendaji wao ili kuwa na uhakika wa magari yetu yanapoenda kufanyiwa matengenezo” alisema mwenyekiti wa halmashauri Mhe. Vumi Magoti. Baraza kwa pamoja liliazimia tija na umuhimu wa uboreshwaji wa utengenezwaji wa magari unaofanywa na TEMESA.

Pamoja na hayo, kwa upande mwingine suala la ujenzi wa stendi ya wilaya lilipata nafasi katika baraza hilo. Stendi ya wilaya ya Busega inayotakiwa kujengwa Nyashimo makao makuu ya halmashauri ya wilaya ya Busega, imeweza kuwa hoja kwenye baraza hilo na madiwani kuomba utekelezaji wake uendane na muda na kwa ufanisi mkubwa kwani ni moja ya chanzo cha kuongeza mapato ya halmashauri.

Mkurugenzi mtendaji wa halmasjauri ya wilaya ya Busega, Anderson Njiginya Kabuko, ameeleza kuwa utekelezaji wa ujenzi wa stendi ya wilaya ipo kwenye utekelezaji wa hatua mbalimbali na taarifa zitazidi kutolewa kutokana na maendeleo ya ujenzi wake.

Kwa upande mwingine suala la ukusanyaji wa mapato ni moja ya mambo muhimu yaliyotajwa na kusisitizwa kuwa na tija kwa ajili ya maendeleo ya halmashauri, hivyo ni muhimu kuwa na vyanzo vingi vya mapato. “Mapato ya halmashauri ni muhimu ndio maana tunajitahidi kuwa na mbinu nyingi ili kupandisha mapato yetu, kwa lengo la kukamilisha shughuli mbalimbali ikiwemo miradi ya maendeleo inayoendelea na iliyopangwa kutekelezwa” alisema mkurugenzi mtendaji, Anderson Njiginya Kabuko.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 12, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa