• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Baraza La Madiwani Busega Lataka Uwepo wa Mahakama ya Wilaya; Lashauri Marekebisho Stendi ya Wilaya; Lahoji Uwezo wa TEMESA

Posted on: June 4th, 2021

Baraza la madiwani halmashauri ya Wilaya ya Busega limetaka uwepo wa Mahakama ya Wilaya Busega. Hayo yamesemwa na wajumbe wa baraza hilo wakati wa kikao cha baraza la madiwani robo ya tatu lililofanyika leo 04 Juni 2021 ukumbi wa Silisos.

Diwani kata ya Nyasimo Mhe. Mickness Mahela amehoji kuhusu suala la uwepo wa Mahakama wilayani Busega, akisema kwamba imekuwa kero kubwa kwa wakazi wa Busega wanapotaka kupata huduma ya mahakama, kwani inawalazimu kwenda Wilaya jirani ya Bariadi kupata huduma hiyo.

“Wilaya ya Busega ina takribani miaka tisa kwasasa, hivyo uwepo wa mahakama ni muhimu kwa wananchi wetu” aliongeza Mhe. Bi. Mickness Mahela. Wajumbe wa baraza hilo wamekiri kwamba uwepo wa mahakama ni suala lisilopingika, huku wakidai kwamba wilaya inahitaji mahakama ili kuondoa kero ya wakazi na wananchi wa Busega.

Akitoa ufafanuzi wa suala la uwepo wa mahakama wilayani Busega, mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa wilaya Busega Bw. David Pallangyo anasema kwamba ni suala ambalo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya imekua ikifuatilia kwa ukaribu na inaendelea na ufutiliaji. Kwa upande mwingine ameeleza kwamba licha ya watumishi wa mahakama kupangiwa kufanyia kazi zao wakiwa Busega lakini bado wanafanyia kazi zao wilayani Bariadi.

Aidha, hoja ya matengenezo ya magari iliibuliwa na wajumbe huku wakitaka uwepo wa gereji ya halmasuri ili kuwa na ufanisi wa matengenezo ya magari hayo kuliko kupeleka magari hayo kwa Wakala wa Ufundi wa Umeme na utengenezaji wa Magari ya Serikali (TEMESA). Akitoa ufafanuzi wa suala hilo Mkurugenzi Mtendaji Bw. Anderson Kabuko licha ya changamoto ya TEMESA, lakini tayari marekebisho na matengenezo madogo yanafanyika kwa baadhi ya magari na kazi hiyo inafanywa na fundi wa halmashauri.

Suala la stendi ya Wilaya ambayo imeanza kufanya kazi mwanzoni mwa mwezi wa tano mwaka huu, pia limepata wasaa wa kujadiliwa na baraza hilo. Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Anderson Kabuko amesema tayari halmashauri imevunja mkataba na mkandarasi wa awali ambae alikuwa akijenga stendi hiyo kutokana na kutofikia ubora wa ujenzi, na tayari utaratibu unafanyika ili kumpata mkandarasi mwingine. Baraza hilo limetaka ujenzi wa wa stendi hiyo uboreshwe hasa njia za kupita magari ili kuondoa usumbufu na kero.

Akiahirisha kikao cha baraza hilo, Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Busega Mhe. Sundi Muniwe, ametaka kuendelea kwa juhudi ujenzi wa stendi ya Wilaya, na kuagiza kwamba kwasasa hatuhitaji mkandarasi, mhandisi wa ujenzi kwa kushirikiana na Meneja wa TARURA kufanya kazi ya ujenzi kuendelea na ujenzi wa stendi ya Wilaya, Nyashimo. Kwa upande mwingine ameomba viongozi wa mkoa kufuatilia suala la mahakama ili wilaya ya Busega iweze kupata mahakama.   

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa