• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
BUSEGA DISTRICT COUNCIL
BUSEGA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Busega

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Dhamira
      • Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utawala na Utumishi
        • Mipango, Takwimu na Ushirika
        • Elimu Msingi
        • Afya
        • Maendeleo ya Jamii na ustawi wa jamii na Vijana
        • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Mifugo na Uvuvi
        • Maji
        • Elimu Sekondari
        • Ardhi na Maliasili
        • Fedha na Biashara
        • Ujenzi na Zimamoto
        • Usafi na Mazingira
      • Vitengo
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Kitengo cha Sheria
        • Kitengo cha Ugavi
        • Uchaguzi
        • TEHAMA na Uhusiano
        • Kitengo cha Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Afya
    • Elimu
    • Maji
      • Kilimo
        • Kilimo
    • Kilimo
      • Kilimo
    • Mifugo
    • uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya, Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya W\heshimiwa Madiwani
        • Kuonana na Mwenyekitiwa Halmashauri
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali za Maombi
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Maendeleo
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KATIBU TAWALA MKOA WA SIMIYU ATAKA MIRADI YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

Posted on: September 10th, 2020

Ukamilikaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wakati kutarahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi. Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Bi. Miriam Mmbaga wakati alipofanya ziara ya kutembelea baadhi ya miradi ya Afya Wilayani Busega tarehe 9 Septemba, 2020, ambapo Bi. Mmbaga aliambatana na Timu ya Usamizi wa Huduma za Afya Ngazi ya Mkoa (RHMT).

Katika ziara hiyo ambayo Mmbaga alitembelea Hospitali ya Wilaya ya Busega ambapo alijionea ujenzi unaoendelea wa Njia za kupita Wagonjwa (Walk Ways) Mita 122 ambao unagharimu zaidi ya TZS Milioni 66.9, na ujenzi wa jengo la Theatre (Upasuaji) na Uzazi wenye thamani ya zaidi ya TZS Milioni 194.3. Mmbaga pia alitembelea ujenzi wa jengo la Upasuaji kituo cha Afya Lukungu, ujenzi unaofadhiliwa na AMREF kwa gharama ya TZS Million 142, na kusisitiza kukamilika kwa jengo hilo kwa wakati ili kuanza kutoa huduma za upasuaji kituoni hapo.  

Kwa upande mwingine Mmbaga ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega kwa kuwa mstari wa mbele katika miradi ya ujenzi wa miundombinu katika Hospitali ya Wilaya ya Busega kwa kuchangia fedha zinazotokana na mapato ya ndani na kumtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega Bw. Anderson Njiginya Kabuko kuendelea na utaratibu huo kwa kuongeza kiasi cha uchangiaji wa fedha. Namshukuru Mkurugenzi kuwa kipaumbele kwenye miradi kwani ameweza kuchangia ujenzi unaondelea na ninamtaka kuongeza zaidi uchangiaji na nampongeza sana, aliongeza Bi. Mmbaga.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Anderson Njiginya Kabuko amemhakikishia Katibu Tawala wa Mkoa kuwa Ofisi yake itaendelea kuchangia fedha ili miradi ikamilike na kuanza kutoa huduma kwa wakati.

Kwa upande mwingine Mmbaga amewataka wafadhili na wadau wa maendeleo kukamilisha miradi wanayofadhili kwa wakati kwani miradi mingi imekuwa ikienda taratibu. Tunajua na tunatambua mchango wa wadau wa sekta ya Afya katika mkoa wetu lakini tunaomba wawe na utaratibu mzuri wa ufadhili wa miradi mbalimbali ili ikamilike kwa wakati, aliongeza Bi. Mmbaga.

Pia Mmbaga amewataka watumishi kuwa na ushirikiano ili kufanikisha huduma bora kwa wananchi. Watumishi mnatakiwa kuwa na ushirikiano ili kufikia malengo ya utoaji huduma, tutumie karama tulizopewa katika ufanyaji kazi, aliongeza Mmbaga. Kwa upande mwingine Mmbaga amempongeza Kaimu Mhandisi wa Ujenzi Wilaya ya Busega, Mhandisi. Paul Tumbu kwa juhudi na bidii ya uchapakazi katika miradi mbalimbali ya ujenzi Wilayani Busega huku akimuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega kufuatilia uthibitisho wa cheo chake ili awe Mkuu wa Idara ya Ujenzi.

Awali Makamu Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Khamis Kulemba amewataka watumishi wa idara ya Afya kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi, na ameipongeza Timu ya Usamizi wa Huduma za Afya wilaya ya Busega (CHMT) kwa kazi nzuri wanayoifanya.  

Katika ziara hiyo pia Mmbaga alitembelea kikundi kinachojihusisha na kilimo cha umwagiliaji kinachojulikana kama Umoja wa Wamwagiliaji Nyakurunduma (UWANYA) na kuwataka wataalam wa kilimo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Busega kushirikiana na kikundi hicho na vingine kwaajili ya kutoa elimu ya uendeshaji na uzalishaji. Pia Mmbaga amevitaka vikundi vya kilimo cha umwagiliaji kutumia vyema rasilimali ya ziwa Viktoria.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA KUANDIKA KWA KADA YA MTENDAJI WA KIJIJI III ULIOFANYIKA TAREHE 05.10.2024 October 05, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi October 07, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba Wilaya ya Busega_2020 November 23, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili December 01, 2020
  • Onyesha zote

Habari Mpya

  • TIJA YA KUONGEZA MAPATO; BUSEGA YATEMBELEA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA KUJIFUNZA MBINU

    April 18, 2024
  • Kamati ya Siasa Mkoa wa Simiyu Yapongeza Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo Busega

    February 24, 2023
  • Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Busega Wapitisha Mapendekezo ya Mpango wa Bajeti Mwaka wa Fedha 2023/2024

    February 14, 2023
  • Mgogoro wa Shamba la Kijiji cha Nyamikoma A uliodumu zaidi ya miaka 15 Wamalizika

    January 11, 2023
  • Onyesha zote

Video za Shughuli za Kiofisi na kitaifa

Stili Picha Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Salary Slip - Salary Slip Portal
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Ajira Portal
  • Wizara ya Mifugo na Uvuvi
  • Wizara ya Nishati
  • Wizara ya Maji
  • Mamlaka ya Chakula na Dawa -TFDA
  • Tovuti ya TRA

Tovuti Mashuhuli

  • Tovuti kuu ya Serikari
  • Tovuti ya menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Tovuti ya Mkoa wa Simiyu
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria
  • Kanzidata, Masuala ya Uchumi na Jamii Tanzania
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Sekretarieti ya Ajira Tanzania
  • Tovuti ya Wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti ya TCRA
  • Tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Tovuti ya Uhamiaji
  • Tovuti ya Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini -RITA
  • Tovuti ya Brela
  • Tovuti ya NIDA
  • Tovuti ya Wakala ya Serikali Mtandao- eGA
  • Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Wilaya ya Busega

    Sanduku la Posta: 157 BUSEGA

    Simu ya Mezani: +255 282 981 193

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@busegadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki @2019. Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Haki zote zimehifadhiwa